STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 15, 2015

Edin Dzeko atua AS Roma toka Etihad

www.bukobasports.com
MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Manchester City Edin Dzeko amejiunga na klabu ya ligi ya Seria A Roma kwa mkopo.
Roma imetoa kitita cha pauni milioni 2.9, na nyingine pauni 7.9 zikitarajiwa kulipwa iwapo uhamisho huo utabadilika na kuwa wa kudumu.
''Nimekuja hapa kushinda mataji'',alisema Dzeko.
''Ninaweza kuahidi kitu kimoja kwamba nitajitahidi vilivyo katika kilabu hii''.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na kilabu ya Etihad kutoka Wolfsburg mnamo mwaka 2011 kwa pauni milioni 27.
Alikuwa ameweka sahihi ya kandarasi ya miaka minne katika uwanja wa Etihad msimu uliopita.
Hatahivyo,meneja manuel Pelegrini hivi majuzi alikiri kwamba Dzeko alikuwa na uwezo mkubwa kuondoka katika Etihad kufutia usajili wa Raheem Sterling kutoka Liverpool kwa kitita cha pauni milioni 49.

No comments:

Post a Comment