STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 15, 2015

Manchester United yafanya kweli Ligi Kuu ya England

Luke Shaw grabs Januzaj after his opening goal put Manchester United on course for their second consecutive victory
Januzaj akishangilia bao lake la wachezaji wenzake wa Man United
MASHETANI Wekundu, Manchester United usiku wa jana walifanikiwa kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza msimu huu baada ya kushinda baoa 1-0 ugenini dhidi ya Aston Villa.
Baoa pekee la dakika ya 29 lililofungwa na Adnan Januzaj limewawezesha vijana wa Louis Van Gaal kushinda mechi ya pili mfululizo katika Ligi Kuu ya England na kukaa kileleni ikiwa na pointi 6.
Pambano hilo lililochezwa Uwanja wa Villa Park, liliwahishwa kuchezwa kutokana na muingiliano wa masuala ya kijamii karibu na mji huo na Mashetani WEkundu wakaona wafanye yao mapema kabla ya kuelekea kwenye pambano lao la mchujo la Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Warusi.
Januzaj alifunga bao hilo akimalizia pasi murua ya Juan Mata. Ligi hiyo itaendelea leo kwa michezo kadhaa, lakini kivumbi kitakuwa kesho kati ya Manchester City dhidi ya mabingwa watetezi Chelsea kwenye Uwanja wa Etihad, mjini Manchester. Tayari makocha wa timu hizo wametoa tambo zaom lakini Manuel Pellegrin amesisitiza ni lazima safari hii ampe mkono Jose Mourinho.

No comments:

Post a Comment