STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 5, 2013

Simba, Golden Bush kupimana ubavu Jumamosi

Kikosi cha Golden Bush
Kikosi cha Kikijifua uwanja wa Kinesi
TIMU isiyofungika ya Golden Bush Fc ya jijini Dar es Salaam inayoshiriki Ligi Daraja la Nne Wialaya ya Kinondoni, wikiendi hii itashuka dimbani kupimana ubavu na Simba inayojiandaa na michuano ya Kombe la Kagame itakayofanyika nchini Sudan.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mlezi wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' pambano hilo la kirafiki ya kujipima nguvu litafanyika siku ya Jumamosi saa 10:30 jioni kwenye uwanja wa Kinesi.
Ticotico alisema mechi hiyo ni muhimu mno kwa vijana wake, lakini pia amemwagia sifa kocha wa Simba, King Abdallah Kibadeni kwa kukubali ombi la timu hizo kupepetana.

Taarifa rasmi ya Golden Bush iliyotumwa na Ticotico kwa blogu hii ni kama ifuatavyo hapo chini;

Naomba nitoe taarifa kwamba siku ya jumamosi weekend hii pale uwanja wa Kinesi timu yetu ya vijana Golden bush itaumana uso kwa uso na Simba sports club kuanzia saa kumi na nusu jioni. ni game ambayo Simba watatumia kama maandalizi yao ya mwishomwisho kwa ajili mashindano ya Kagame Cup huku Golden bush tukitumia game hiyo kungalia vijana wetu wameiva kiasi gani ajili ya mzunguko wa pili wa ligi daraja la nne Kinondoni. tunawaomba mashabiki, wapenzi, wadau, wakereketwa tufike Kinesi jumamosi jioni ili tushuhudie mpambano wa kutaka na shoka.

Aidha nichukue nafasi hii kumpongeza King Kibadeni kwa kukubali game yetu bila mizengwe, ikumbukwe kwamba King ndiye alifanikisha game yetu na Kagera sugar wakati ule akiwa kocha wao. juzi tena Uongozi umeomba game na bila ajizi King kasema kipigwe siku ya jumamosi.

Najua veterans watakuwa na game weekend hii na kama itakuwa jumamosi basi mkae mkao wa kula maana Golden bush tutao burudani asubuhi na jioni, kwa kiswahili unapiga nyuma na mbele.

naomba kutoa hoja.

No comments:

Post a Comment