STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 5, 2013

Mabondia Francis Miyeyusho,Mashali kupamba usiku wa matumaini Taifa


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEinRhjpHSbCg9922iuKEu7yRGuZPivlZYKf5raXPv4zYh46zFQoJQ0-1Sh6iLAKEVHIbv3u3aFQ0lHTdlr_OU9lIuCGjNoDBHEDotXfejWXg0vtj6VvPMB_uhMfTLKiCj0cwmyJUrBGp-GB/s640/miyeyusho3.JPG
Francis Miyeyusho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgtcm3L7pzcbja7bSnx_bJy-ImxGoBHRqZqfw5QUsg3g5ocnIaLOkRpz-LEPJGDUySKvqg1G_zJ11McXXzRECzzEm3xIIYxJrvk0zRrkugyCJ2Hx9PHrLbn-wMfi2SGRUeXMUb8SU9J0cg/s1600/IMG_5146.JPG
Thomas Mashali

MABONDIA nyota nchini Francis Miyeyusho na Thomas Mashali wanatarajiwa kupigana na mabondia kutoa nchi jirani za Kenya na Uganda katika kulinogesha Tamasha la Usiku wa Matumaini linalotarajiwa kufanyika Julai 7 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo litakalofanyika kwa mara ya pili tangu kuanzishwa kwake linaratibiwa na kampuni ya Global Publishers na litasimamiwa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO).
Akizungumza na MICHARAZO, Rais wa TPBO-Limited, Yassin Abdallah 'Ustaadh' alisema  Miyeyusho bingwa wa Afrika wa uzani wa Bantam na Mashali bingwa wa Afrika Mashariki na Kati uzito wa Kati ndiyo watakaopamba usiku huoi utakaokuwa na burudani mbalimbali siku hiyo.
Ustaadh alisema mabondia hao wa Tanzania watapanda ulingoni siku hiyo kwenye uwanja wa Taifa kuzipigana na mabondia kutoka Kenya na Uganda ambao majina yao yatarajaiwa kuanikwa hivi karibuni.,
"Tumewateua mabondia Francis Miyeyusho na Thomas Mashali ili waweze kupambana na mabondia toka nje ya nchi kati ya Kenya na Uganda na kwa sasa tunaendelea na mawasiliano na vyama vya mchezao huo vya nchi hizo ili kupata majina ya wapinzani wa mabondia wetu," alisema Ustaadh.
Ustaadh alisema mabondia hao wa Tanzania hawatawaangusha Watanzania siku ya tamasha hilo ambalo mwaka jana lilishuhudiwa bondia Francis Cheka akimkimbia kwenye ulingo, bingwa wa Taifa wa PST, Japhet Kaseba.
Kama ilivyokuwa mwaka jana tamasha hilo la 'Night of Hope', lina lengo la kusaka fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni kwa wanafunzi wa kike nchini.

No comments:

Post a Comment