STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 5, 2013

Uchaguzi Mkuu wa BFT sasa Julai 7


Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga
UCHAGUZI Mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT) ambao awali ulitangazwa ungefanyika mwishoni mwa Mei, sasa umepangwa kufanyika Julai 7, jijini Mwanza.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolea na BFT ikisainiwa na Katibu Mkuu wake, Makore Mashaga uchaguzi huo ufanyika sambamba na michuano ya Majiji ambayo nayo iliahirishwa mpaka Julai badala ya Mei kama ilivyokuwa imepangwa.
Taarifa hiyo inasema kuwa nafasi zitakazowaniwa katika kinyang'anyiro hicho ni Urais, Makamu wake, Katibu Mkuu, Mhazini na Wajumbe 9 wa Kamati ya Utendaji wa shirikisho hilo zitakazohusisha Kamati za Mipango na Fedha, Waamuzi na Majaji, Mashindano na Vifaa, Walimu, Ufundi na Utafiti, Kamati ya Uhusiano, Habari na Masoko,  Wanawake, Kamati ya Maendeleo ya Mikoa na Taasisi za Umma.
Kamati ya Tiba na Kamati za Maendeleo ya Vijana na Wachezaji.
Fomu za uchaguzi huo zimeshaanza kutolewa tangu leo Jumanne (04/06/2013) katika Ofisi za Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na zoezi litaendelea hadi Julai 7, ambapo ada za fomu hizo zimepangwa kulingana na nafasi ambayo mgombea atajitokeza kuiwania.
Kwa fomu ya kuwania nafasi ya Rais, ada yake ni Tsh. 150,000/=, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu na Mweka Hazina kila moja ni Tsh. 100,000/=, wakati kwa nafasi ya Ujumbe kila fomu itauzwa kwa Tsh. 50,000/=
BFT imetoa wito kwa  watanzania wenye uwezo wa kuongoza michezo kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu za kugombea nafasi kama zilivyoelezwa hapo juu.

No comments:

Post a Comment