STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 30, 2016

Juanfran wa Atletico Madrid aomba radhi mashabiki

http://www.101greatgoals.com/wp-content/uploads/2016/05/Juanfran-Atletico-Madrid.jpgBAADA ya kukosa penalti katika mechi ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya mahasimu wao, Real Madrid, beki wa Atletico Madrid Juanfran Torres amewaomba radhi mashabiki wa klabu hiyo.
Beki huyo wa kulia aliyefunga penati ya ushindi katika hatua ya 16 Bora dhidi ya PSV Eindhoven ndiye aliyekuwa mchezaji pekee wa Atletico aliyekosa penalti kwenye Uwanja wa San Siro, Milan Italia wakati wa mikwaju ya penalti na kusaidia kuipa Real Madrid taji la 11 baada ya Cristiano Ronaldo kufunga ya mwisho.
Real Madrid  ilishinda kwa penalti 5-3 baada ya kumaliza dakika 120 timu zote zikifungana bao 1-1, huku Antonie Griezmann akipoteza penalti ambao ingeweza kuisawazishia Atletico katika kipindi cha kwanza.
Juanfran walitia simanzi akiwashinda wachezaji wenzakwa kwa huzuni kubwa iliyowapata baada ya matokeo hayo na beki huyo amewaomba radhi mashabiki wao kwa kile kilichotokea.
Leo Jumatatu Juanfran ameaandika barua maalum kwa mashabiki wa Atletico Madrid ili kuwaomba radhi kwa kilichotokea. Barua hiyo imetupiwa pia katika akaunti ya klabu hiyo ya Instagram.

Waraka huo  unasomeka hivi;


http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/05/Juanfran.jpg
Wakara huo wa Juanfran

 
Hello Atleticos,

Nimeomba klabu kuwafikishia barua juu ya kila kitu ninachojisikia
Kamwe sitasahau moyo wa dhati mlioonesha kwangu wakati nilipokuja kwenu kuomba msamaha. Nikiona machozi yangu yakitiririka mbele ya maelfu ya mashabiki wa Atletico waliofika uwanjani na kunisaidia kuendana na uhalisia wa huzuni kubwa iliyokuwa imejaa kwenye nafsi yangu. Vile vile bila ya kusahau sapoti niliyopata kutoka kwa wachezaji wenzangu, kocha na watu wote wanaounda familia hii ya Atletico.
Pia ningependa kuwashukuru kwa imani kubwa ambayo mara zote mmekuwa mkionesha kwetu na zaidi ya yote ni kutufanya sisi kujiona watu wa tofauti wengine na wenye nafsi ya kipeke kutokana na uwepo wetu hapa Atletico.
Miaka miwili iliyopita, niliwaambia kwamba tungerejea tena fainali na tumefanya hivyo, sasa, nawaambia kwamba, Gabi, nahodha wetu hivi karibuni au baadaye atanyanyua Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya na kusherehekea sote kwa pamoja.
Nawapenda sana na tusonge mbele Wana-Atletico.

No comments:

Post a Comment