KWA HABARI ZA BURUDANI, MICHEZO NA MATUKIO MBALIMBALI
STRIKA
USILIKOSE
Monday, May 30, 2016
JT amuunga mkono Mourinho Man United
NAHODHA wa Chelsea John Terry amemuunga mkono Jose Mourinho kufanikiwa kwenye
Klabu yake mpya Manchester United huku akimueleza kuwa Meneja huyo ndie
bora kupita yeyote aliewahi kucheza chini yake. Terry alikaribia
kuondoka Chelsea mwishoni mwa Msuimu huu baada ya Mkataba wake
kumalizika lakini sasa ameongezewa Mwaka Mmoja na Msimu ujao atakuwa
chini ya Meneja mpya wa Chelsea Antonio Conte ambae ni Meneja wa sasa wa
Timu ya Taifa ya Italy. Terry,
ambae aliteuliwa na Mourinho kuwa Kepteni wa Chelsea wakati Mourinho
alipotua Chelsea kwa mara ya kwanza Mwaka 2004, ameeleza: “Ni habari
njema kwa Manchester United. Hii itawafurahisha Mashabiki na Wachezaji
wa Man United kwani mara nyingi nimesema Mourinho ndie Meneja Bora
niliyewahi kufanya nae kazi!”
No comments:
Post a Comment