STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 30, 2016

Huyu dogo, Rashford acha kabisa Man United

KINDA wa Manchester United, Marcus Rashford aliyeibuka msimu huu na kuwa Staa amezawadiwa mkataba mpya ulioboreshwa.
Straika huyo, 18 alisaliwa na mwaka mmoja tu kwenye mkataba wake wa sasa, lakini sasa atapewa mkataba mpya wa muda mrefu na kuzoa Pauni 20,000 kwa wiki.
Wikiendi Rashford, akiichezea England kwa mara ya kwanza kabisa, alifunga bao katika sekunde 138 tu tangu mpira wakati England inaichapa Australia 2-1 na kuweka rekodi kuwa kijana mdogo kabisa kuifungia England katika mechi yake ya kwanza.
Rashford aliibuka Msimu huu kuchezea Man United alipochezeshwa kwa mara ya kwanza Timu ya kwanza dhidi ya FC Midtjylland kwenye Europa Ligi na kupiga Bao 2 na kisha tena kupiga Bao 2 walipocheza na Arsenal kwenye Ligi Kuu England.

Tangu wakati huo, katika Mechi 18 za Man United, Rashford amepiga Bao 8.
Mbali ya Rashford, Kijana mwingine wa Man United ambae nae amebakisha Mwaka mmoja na atapewa Mktaba mpya bora na mrefu ni Cameron Borthwick-Jackson.

No comments:

Post a Comment