STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 30, 2016

Rashford asaini mkataba mpya mrefu Man United

http://ichef.bbci.co.uk/onesport/cps/800/cpsprodpb/ECD9/production/_89833606_marcus_rashford_cameron_borthwick_jackson.jpg
Rashford kushoto na kinda mwenzake Cameron Borthwick-Jackson wakisaini mikataba yao mipya ndani ya Man United
YAMETIMIA. Straika chipukizi wa Manchester United, Marcus Rashford amesainishwa mkataba mpya utakaoenda hadi Juni 2020.
Mkataba huo umeenda sambamba na kuongezwa kwa mshahara wake kwa wiki ambao sasa atalamba Pauni 20, 000, kitu ambacho kinda huyo ameeleza kufurahishwa nacho.
Rashford amejizolea umaarufu mkubwa katika mechi chache za Man United katika Ligi Kuu ya England na michuano ya UEFA Europa League kwa kuifungia mabao na juzi Jumapili aliandikisha rekodi ya kuwa mchezaji kinda kufunga katika kikosi cha Three Lions akicheza mechi yao ya kwanza kabisa.

Zoezi hilo la kusaini mkataba mpya lilienda sambamba pia kwa chipukizi mwingine, Cameron Borthwick-Jackson ambaye naye atajibanza Man United mpaka 2020.

No comments:

Post a Comment