STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 27, 2016

Dani Alves ainyima ubingwa Real Madrid Ulaya

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2016/05/17/16/344C8FAD00000578-0-image-a-60_1463500208098.jpg
Dani Alves
https://cdn2.vox-cdn.com/thumbor/7-e7Hp4ZSgo6fGmgV0DLxHNGWuQ=/0x25:3000x2025/1310x873/cdn0.vox-cdn.com/uploads/chorus_image/image/49093871/GettyImages-515165792.0.jpg
Atletico Madrid
KUELEKEA kwenye Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itakayochezwa kesho Jumamosi, Beki wa Barcelona, Dani Alves amekiri kuwa angependelea zaidi Atletico Madrid ishinde taji hilo kuliko mahasimu wao Real Madrid.
Atletico na Madrid zitavaana kesho, katika mechi ya kisasi kwea kocha Diego Simeone ambaye alifungwa kwenye fainali ya mwaka juzi na mabingwa hao wa kihistoria wa michuano hiyo ya Ulaya kwa mabao 4-1.
Atletico walio chini Diego Simeone ndio waliowang’oa mabingwa watetezi Barcelona katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kabla ya kuitoa tena Bayern Munich kwenye hatua ya nusu fainali.
Madrid ndio timu pekee iliyopo mbele ya Atletico kwasasa ikiwa ni kama marudiano baada ya ile fainali ya mwaka 2014 ambapo Madrid waliibuka kidedea kwa kushinda mabao 4-1 katika muda wa nyongeza.
Hata hivyo, Alves ana mawazo tofauti katika fainali hiyo itakayofanyika katika Uwanja wa San Siro jijini Milan nchini Italia kwani anadhani Atletico wanastahili zaidi taji hilo kuliko Madrid. Alves amesema Atletico ni timu ambayo imepambana sana mpaka kufikia hapo walipo hivyo anadhani wanastahili taji hilo

No comments:

Post a Comment