STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 27, 2016

Jose Mourinho atambulishwa rasmi Man United

Jose Mourinho poses with a Manchester United shirt after being confirmed as the club's new manager
Jose Mourinho akitua rasmi Man United
YAMETIMIA. Hatimaye klabu ya Manchester United imemtangaza na kumtambulisha rasmi Kocha Jose Mourinho kuwa kocha wao mkuu na kumpa kandarasi ya miaka mitatu.
Mourinho, mwenye miaka 53 ametangazwa na klabuni na kuchapishwa picha akiwa na jezi za klabu yake mpya ambayo ilikuwa ikimsaka tangu alipotemwa Chelsea katikati ya msimu uliomalizika wa EPL.
Kocha huyo alisaini mkataba huo jana jioni baada ya mazungumzo ya siku tatu kabla ya kutambulishwa akiwa kavalia suti kali nyeusi jambo linaloashiria kuwa, Special One sasa ni mali ya Mashetani Wekundu na wapinzani wao wajipange kwa mikakati anayokuja nayo kocha huyo mjuzi.
Moja ya mikakati inayotajwa kuwa mikononi mwa Mourinho ni kumnyakua Willian anayekipiga Chelsea ambaye alinunuliwa na kocha huyo wakati akiinoa klabu hiyo ya The Blues.

No comments:

Post a Comment