STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 27, 2016

Juventus kumng'oa Mascherano Nou Camp

http://ghettoradio.co.ke/wp-content/uploads/2015/10/javier-mascherano.jpgMABINGWA wa Italia, Juventus imepanga kumng'oa Kiungo mahiri wa Barcelona, Javier Mascherano.
Inadaiwa kuwa Muargentina huyo amekubali dili la kujiunga na mabingwa wa Serie A.
Duru za kimichezo zinasema kuwa, nyota huyo wa kimataifa wa Argentina amefanya mazungumzo na Juventus na anajiandaa kuhamia jijini Turin kiangazi hiki.
Mpaka sasa inadaiwa kuwa hakuna makubaliano yoyote kati ya Barcelona na Juventus na mabingwa hao wa Hispania wanahisiwa kutokuwa na mpango wowote wa kumuachia kiungo huyo mwenye umri wa miaka 31.
Mascherano alijiunga na Barcelona mwaka 2010 akitokea Liverpool na kufanikiwa kushinda mataji manne ya La Liga na mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa Camp Nou.

No comments:

Post a Comment