STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 22, 2016

HIVI NDIVYO LIGI KUU BARA 2015-2016 ILIVYOISHA RASMI

Mabingwa Yanga

Simba washindi wa tatu
Majimaji iliyoigomea Yanga mjini Songea
PAZIA la Ligi Kuu Bara limefungwa rasmi jioni hii ikishuhudia timu tatu za jijini la Tanga, Coastal Union, African Sports na Mgambo JKT zikishuka rasmi kwa kushika nafasi tatu za chini, huku Simba ikishindwa kuvunja mwiko wa kukamata nafasi ya pili tangu ilipotwaa ubingwa wake wa mwisho wa Ligi Kuu msimu wa 2011-2012 ikizidiwa ujanja na Azam.
Sports maarufu kama Wana Kimanumanu walilala mabao 2-0 mbele ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Manungu Complex, Turiani Morogoro, wakati Wagosi wa Kaya Coastal ikilala tena mabao 2-0 Mkwakwani Tanga mbele ya Prisons-Mbeya licha ya kwamba ilishashuka mapema katika ligi hiyo.
Mgambo JKT ilishindwa kukomaa kujiokoa kama misimu mitatu iliyopita ilivyopambana baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Azam na kujikuta pointi zake kutotosha kuiokoa isirudi Ligi Daraja la Kwanza baada ya kucheza mfululizo tangu ilipopanda mwanzoni mwa miaka ya 2010.
Simba ikiwa Uwanja wa Taifa ilishindwa kuhimili vishindo vya JKT Ruvu na kulala mabao 2-1 ikiiacha Azam ikitwaa zawadi ya mshindi wa pili nyuma ya Yanga ikiwa msimu wa tano mfululizo kwa Wanalambalamba kutotoka kwenye Mbili Bora ya ligi hiyo tangu mwaka 2011-2012.
Mjini Songea Majimaji ikiwa Uwanja wake wa Majimaji, ililazimishwa sare ya mabao 2-2 na Mabingwa Yanga, huku ikishuhudiwa Ally Mustafa Barthez akifunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu, huku Paul Nonga akiifungia Yanga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu tangu aliposajiliwa katika dirisha dogo mwishoni mwa mwaka jana.
Toto Africans imenusurika kushuka daraja licha ya kufungwa bao 1-0 na Stand United Uwanja wa CCM Kirumba, kama ambavyo Kagera Sugar ilivyoponea kwa Wana Shinyanga wengine Mwadui FC waliowazabua mabao 2-0.
Mbeya City ikiwa nyumbani ilishindwa kulipa kisasi cha kufungwa mabao 4-1 na Ndanda katika mchezo wao wa kwanza mjini Mtwara kwa kutoka suluhu kwenye Uwanja wa wa Sokoine, Mbeya.
Kwa namna msimamo ulivyo, Yanga iliyotwaa ubingwa mbali na kunyakua Kombe na Medali, pia imevuta mkwanja upatao Sh. 81,345,723/= kama washindi wa kwanza, wakati Azam  ikizoa Sh. 40,672,861/= za ushindi wa pili.
Simba yenyewe imevuta donge la Sh. 29,052,044/= kwa kushika nafasi ya tatu wakati Prisons iliyokuwa ya nne ikiipiku Mtibwa Sugar imeweka kibindoni Sh. 23,241,635/=
Kadhalika kumalizika kwa ligi hiyo kumempa nafasi Amissi Tambwe wa Yanga kuibuka kinara wa mabao msimu huu akifunga jumla ya 21 na kujihakikishia zawadi ya Sh. 5,742,940/= mbele ya Hamis Kiiza wa Simba aliyekuwa akiongoza kwa muda mrefu kabla ya kupoteza makali yake.

Matokeo kamili na msimamo wa mwisho wa Ligi hiyo ni kama ifuatavyo;



Msimamo wa Ligi Kuu Bara:

                            P  W   D   L   F    A  Pts

1. Yanga               30 22  7   1  70  20  73

2. Azam                30 18 10  2  47  24 64

3. Simba               30 19  5   6  45  17 62

4. Prisons              30 13 12  5  29  22 51

5. Mtibwa              30 14  8   8  33  21 50

6. Mwadui FC         30 11  8  11 29  29 41

7. Stand Utd          30 12  4  14 28  29 40

8. Mbeya City        30  9   8  13 32  34 35

9. Ndanda             30  7  14  9  28  31 35

10.Majimaji           30  9   8  13 22  40 35

11.JKT Ruvu          30  8   8  14 31  43 32

12.Toto Africans     30  7   9  14 26  40 30

13.Kagera Sugar    30  8   7  15 23  34 31

14.Mgambo           30  6  10 14 24  36 28

15.African Sports   30  7   5  18 13  34 26

16.Coastal Union    30  5  7   18 15  41 22
 
Wafungaji: 
 
21-Amissi Tambwe               (Yanga)
19-Hamis Kiiza                      (Simba)
17-Donald Ngoma                (Yanga)
16-Jeremiah Juma               (Prisons)
15-Elias Maguli                      (Stand)
12- Kipre Tchetche                 (Azam)
10-John Bocco                       (Azam)
     Atupele Green              (Ndanda)
9-  Ibrahim Ajib                     (Simba)
     Shiva Kichuya               (Mtibwa) 
     Simon Msuva                  (Yanga)
 8- Shomary Kapombe          (Azam)
     Fully Maganga            (Mgambo)
 
7- Mbaraka Yusuf              (Kagera) 
    Mussa Kiumbu           (JKT Ruvu)
    Waziri Junior                     (Toto)
       Saady Kipanga          (JKT Ruvu) 
6- Danny Mrwanda         (Majimaji) 
  
  AbdulRahman Mussa (JKT Ruvu)
5-Said Bahanuzi               (Mtibwa)
    Samuel Kamuntu       (JKT Ruvu)
    Miraji Athuman                  (Toto)
    Jerry Tegete                 (Mwadui)
    Thabani Kamusoko         (Yanga)
    Mohammed Mkopi      (Prisons)
    Raphael Alpha                (Mbeya)
    Didier Kavumbagu           (Azam)
   Paul Nonga                       (Yanga)

4- Aziz Gillah                   (Mgambo)
    Juma Abdul                      (Yanga)  
    Edward Christopher         (Toto)
3- Michael Aidan            (JKT Ruvu)
    Haruna Moshi                (Mbeya)
    Pastory Athanas              (Stand)
    Adam Miraj                    (Coastal)
    Kiggy Makassy             (Ndanda)
    Omar Mponda             (Ndanda)
    Peter Mapunda           (Majimaji)
   Danny Lyanga                 ( Simba)
   Babu Ally                        (Kagera)
   Mzamiru Yasin               (Mtibwa)
   Bryson Raphael            (Ndanda)
   Joseph Mahundi            (Mbeya)
   Deus Kaseke                  (Yanga)
   Mudathir Yahya              (Azam)
   Kelvin Sabato              (Mwadui)
   Alex Kondo                   (Ndanda) 
2-Malimi Busungu              (Yanga)
   Ally Myovela                 (Prisons)
   Mohamed Ibrahim       (Mtibwa)
   Ally Shomary                (Mtibwa)
   Fabian Gwanse             (Mwadui)
   Jabir Aziz                      (Mwadui)
   Nassor Kapama             (Coastal)
   Thabit Khamis            (JKT Ruvu)
   Frank Domayo                  (Azam)
   Abslim  Chidiebele       (Coastal)   
   Hamad Mbumba            (Sports)
   Ditram Nchimbi     (Mbeya City)
   Kassim Selembe               (Stand)
   Nizar Khalfan                (Mwadui)
   Juma Mahadhi              (Coastal)
   Paul Ngway                    (Kagera)
   Farid Mussa                      (Azam) 
   Japhet Mkala                     (Toto)
   Chande Magoya         (Mgambo)
   Ally Ramadhani               (Sports)
   Salum Kabunda             (Mwadui)
   Kelvin Yondani                 (Yanga)  
   Salim Mbonde              (Mtibwa)
   Abdallah Juma              (Mbeya)
   Stamili Mbonde          (Majimaji)
   Omar Issa                        (Sports)
   Jumanne Alfadhil          (Prisons)
   Hassan Materema         (Sports)
   Frank William                (Prisons)
   Bolly Ajali Shaibu        (Mgambo) 
   Jaffar Ramadhani             (Toto)

No comments:

Post a Comment