STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 22, 2016

Tanga ndio basi tena Ligi Kuu msimu ujao

Mgambo JKT

Africans Sports

Coastal Union
KLABU za Mgambo JKT na Africans Sports zimeungana na Coastal Union kushuka daraja msimu huu ikiwa ni rekodi kwa mkoa mmoja kupoteza timu tatu kwa mpigo katika msimu mmoja.
Sports imelala mabao 2-0 mbele ya Mtibwa Sugar, wakati Mgambo imeambulia sare ya bao 1-1 ambayo imeshindwa kuwabeba mbele ya Azam, na Coastal iliyoshuka mapema ikikubali tena kipigo cha bao 1-0 mbele ya Prisons uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Matokeo ya mwisho ya mechi za kufungia msimu tutawaletea hivi punde, lakini ni kwamba Simba imelala mabao 2-1 mbele ya JKT Ruvu na kushindwa kunyakua nafasi ya pili iliyoenda kwa Azam kwa msimu wa tano mfululizo sasa.

No comments:

Post a Comment