STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 22, 2016

Van Gaal aaga Man Utd kumpisha Mourinho

http://i2.manchestereveningnews.co.uk/incoming/article10144211.ece/ALTERNATES/s615/JS73121391.jpg
Picha haihusiani na taarifa hii. KOcha Louis Van Gaal
KOCHA Mkuu wa Man United, Louis Van Gaal aliyeisaidia klabu hiy9o kunyakua ubingwa wa Kombe la FA usiku wa jana kwa kuilaza Crystal Palace katika pambano la fainali lililochezwa dakika 120, ameaga rasmi Old Trafford kuashiria anampisha Jose Mourinho kuja kuinoa timu hiyo.
LVG ametoa kauli hiyo mchana huu akizungumza katika mkutano wake na wanahabari hotelini kwa kusema kuwa imetosha, ikiwa ni kama kuweka wazi kuwa anaondoka OT.
Kocha huyo amekuwa na wakati mgumu katika klabu hiyo, mashabiki wakitaka asepe zake kwa kushindwa kuirejesha klabu yao katika heshima kama ilivyokuwa chini ya Sir Alex Ferguson aliyestaafu miaka michache iliyopita.
Jose Mourinho amekuwa akitajwa kumrithi Mholanzi huyo, huku taarifa za jana zilikuwa zikidai kuwa, huenda LVG akawa Mkurugenzi wa Ufundi wa Man United, lakini kwa kaul;i aliyotoa mchana huu ni wazi, ndio basi tena.

No comments:

Post a Comment