MSHAMBULIAJI nyota wa Italia, Super Mario
Balotelli amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Liverpool kwa pauni
milioni £16 akitokea AC Milan kwa mkataba wa miaka mitatu na kukabidhiwa jezi namba 45.
Balotelli, 25 alitua mchana wa jana Melwood na kumalizana na uongozi wa Liverpool kabla ya kusaini mkataba huo na kukabidhiwa jezi yenye namba hiyo ambayo amekuwa akitumia kuanzia Manchester City na AC Milan alikotokea kwa sasa.
Alifanyiwa ukaguzi wa afya na mtaalamu wa mambo ya utabibu wa Liverpool Ryland Morgans.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester City atakuwa akilipwa kwa wiki kiasi cha pauni £125,000 ndani ya uga wa Anfield,
alihudhuria pambano la usiku wa jana dhidi ya Manchester City, ambapo klabu yake mpoya ilinyukwa na ile aliyoichezea kabla ya kwenda Milan.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Italia Balotelli akiweka pozi
mbele ya kikombe cha Ulaya ambacho Liverpool imetwaa mara tano huku mara
ya mwisho ikiwa ni 2005

Balotelli akiwa amepozi pembeni ya nembo ya klabu yake mpya ya Liverpool.

Balotelli akisaini mkataba wa kuichezea Liverpool akiwa anarejea England baada ya miezi 18 kupita tangu aondoke Manchester City kwenda AC Milan na kuifungia mabao 30.


No comments:
Post a Comment