STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 26, 2014

Mario Balotelli akabidhiwa namba ile ile 45

MSHAMBULIAJI nyota wa Italia, Super Mario Balotelli amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Liverpool kwa pauni milioni £16 akitokea AC Milan kwa mkataba wa miaka mitatu na kukabidhiwa jezi namba 45.
Balotelli, 25 alitua mchana wa jana Melwood na kumalizana na uongozi wa Liverpool kabla ya kusaini mkataba huo na kukabidhiwa jezi yenye namba hiyo ambayo amekuwa akitumia kuanzia Manchester City na AC Milan alikotokea kwa sasa.
Alifanyiwa ukaguzi wa afya na mtaalamu wa mambo ya utabibu wa Liverpool Ryland Morgans.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester City atakuwa akilipwa kwa wiki kiasi cha pauni £125,000 ndani ya uga wa Anfield, alihudhuria pambano la usiku wa jana dhidi ya Manchester City, ambapo klabu yake mpoya ilinyukwa na ile aliyoichezea kabla ya kwenda Milan.
History makers: Italian striker Balotelli poses with the European Cup, which Liverpool have won five times, most recently in 2005
Mshambuliaji wa kimataifa wa Italia Balotelli akiweka pozi mbele ya kikombe cha Ulaya ambacho Liverpool imetwaa mara tano huku mara ya mwisho ikiwa ni 2005
Ready for business: The 24-year-old arrived at Melwood on Monday afternoon to put the finishing touches to the transfer
Balotelli  akiwa amepozi pembeni ya nembo ya klabu yake mpya ya Liverpool.
Signing up: Balotelli returns to England after an 18-month absence having scored 30 goals with AC Milan
Balotelli akisaini mkataba wa kuichezea Liverpool akiwa anarejea England baada ya miezi 18 kupita tangu aondoke Manchester City kwenda AC Milan na kuifungia mabao 30.
Raring to go: Balotelli poses in the boot room at Melwood, and will be in attendance for Liverpool's clash with Manchester City on Monday
'A great team with young players': Balotelli, who left Manchester City in 2013, said Liverpool are one of the best teams in England

No comments:

Post a Comment