STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 26, 2014

Liverpool yamkaribisha Balotelli kwa kichapo


Balotelli akiishuhudia Liverpool ikilala Etihad kwa mabao 3-1
http://img.theepochtimes.com/n3/eet-content/uploads/2014/08/22/453741350-676x450.jpg
Kun Aguerro akishangilia bao lake walipoifumua Liverpool mabao 3-1
VIJANA wa Brendan Rogers, Liverpool wamemtambulisha mshambuliaji wao nyota kutoka AC Milan , mario Balotelli, wamejikuta wakipata kipigo cha mabao 3-1 ugenini mbele ya mabingwa watetezi Manchester City katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Machester City ni kama ilimkaribisha tena Balotelli kwenye dimba la Etihad kwa kuwaonyesha kuwa wao ni zaidi kwa ushindi huo ambao umeifanya timu hiyo kujogea kwenye nafasi za juu za msimamo wa ligi hiyo iliyomaliza raunid mbili za awali.
Mabao mawili ya Stevan Jovetic na jingine la Sergio 'Kun' Aguerro yalitosha kuwazima vijogoo vya Anfield ambao wanahaha kusaka mbadala wa mshambuliaji wao nyota waliyemuuza Barcelona, Luis Suarez.
Liverpool ingeondoka patupu Etihad kama siyo beki wa City Zabaleta kujifunga na kuwaoa bao la kufutia machozi na kuwapa wakati mgumu kujiandaa kuwakabili Tottenham Hotspur ambao wanaoongoza msimamo kwa sasa japo wanalinda pointi na Chelsea na City walioruhusu nyavu zao kufungwa bao moja tofauti na Spurs ingawa zote zina pointi 6 na mabao matano ya kufunga.

No comments:

Post a Comment