STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 25, 2014

Samuel Eto'o ajiandaa kutua Everton

http://www.foci-live.hu/files/2014/05/samuel-etoo-chelsea1.jpgBAADA ya Liverpool kumpotezea na kuamua kumsajili Mshambuliaji mtukutu kutoka AC Milan, Mario Balotelli, Mcameroon, Samuel Eto'o anajiandaa kutua kwa mahasimu wa Liverpool, Everton imethibitika.
Eto'o aliye huru baada ya kumaliza mkataba wake wa mwaka mmoja na Chelsea, inaelezwa yupo hatua ya mwisho kutua kwa kikosi cha kocha Roberto Martinez.
Nyota huyo wa zamani wa klabu za Real Madrid, Barcelona, Inter Milan na Chelsea, alikuwan akitajwa kuelekea Anfield baada ya Jose Mourinho kumchunia Stamford Bridge.
Mshindi huyo wa tuzo ya klabu bingwa Ulaya, Eto’o amekuwa akihusishwa na vilabu kadhaa kiangazi hii lakini taarifa za hivi punde zinaonekana wazi kuwa Everton maarufu kama Toffees wameshindwa mbio za kupata huduma yake.
Eto'o 33 amehifadhi rekodi nzuri ya kufunga zaidi ya magoli 300 na Martinez anataka mtu wa kutumainiwa nyuma ya mshambuliaji wake Romelu Lukaku.
Arouna Kone amekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na kuwa majeruhi na bado ataendelea kukosekana ilhali Steven Naismith akiwa ndio mshambuliaji namba mbili.
Eto’o atalazimika kupunguza kiasi cha malipo anayotaka cha pauni £130,000 kwa wiki endapo atakabidhiwa mkataba wa miaka miwili ambao inaonekana ni kama Everton imefanya usajili kwa fedha fedha nyingi msimu huu wa uhamisho.

No comments:

Post a Comment