STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 25, 2014

Stars kukipiga na Morocco kirafiki tarehe ya FIFA

http://tff.or.tz/wp-content/uploads/2014/05/taifa-stars-2014.jpgTIMU ya soka ya taifa, Taifa Stars kitasafiri mpaka Morocco kwenda kucheza na wenyeji wake katika mechi ya kirafiki ndani ya tarehe za Fifa.
Mechi hiyo imepangwa kuchezwa Septemba 5 nchini Morocco. Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Mwesigwa Celestine amesema wamepokea mwaliko na tayari Kocha Mart Nooij ameishatangaza kikosi chake.
"Ni tarehe ambayo iko ndani ya tarehe za Fifa, hivyo maandalizi yanaanza na kocha ameishaita kikosi," alisema Mwesigwa ambaye pia ni katibu mkuu wa zamani wa Yanga.
Katika mechi yake ya mwisho, Stars ilichapwa kwa mabao 2-1 ikiwa ugenini nchini Msumbuji na kutolewa katika mbio za kuwania kucheza michuano ya Mataifa Afrika.

No comments:

Post a Comment