STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 25, 2014

Chriss Brown anusurika kufa kwa risasi Marekani

Chris Brown aliyenusurika kuchapwa risasi
http://www.vibe.com/sites/vibe.com/files/styles/article-bounds-718/public/photo_gallery_images/suge-knight-crazy-quotes.jpg
Suge Knight aliyejeruhiwa kwa risasi mbili
MUIMBAJI nyota wa Marekani Chris Brown amenusurika kuuawa katika shambulio la risasi ndani ya klabu ya usiku jijini Los Angeles ambapo prodyuza Suge Knight amejeruhiwa.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo katika klabu ya usiku iitwayo 1OAK iliyopo magharibi mwa Hollywood wakati wa shoo iliyokuwa ikiongozwa na Cris Brown kabla ya zoezi la utoaji Tuzo za VMA ambapo watu watatu wamejeruhiwa mmoja akiwa mahututi.
Suge Knight alipigwa risasi mara mbili tumboni na mkononi na kukimbizwa hospitali ambapo anaendelea na matibabu.
Mastaa wengine waliokuwepo kwenye klabu hiyo wakati tukio hilo likitokea ni pamoja na Justin Bieber, rappa The Game, Pia Mia, Tyson Beckford, Robert Ri'chard  na wengineo.
Indaiwa mlengwa mkuu katika shambulio hilo alikuwa Chris Brown, lakini Mungu akamuepushia msala huo unaokumbusha matukio ya nyota wa hiphop 2 Pac Shakur na BIG Notorious waliouwawa katika mikasa tofauti ya ulipizaji kisasi baina ya kambi za East Coast and West Coast

No comments:

Post a Comment