STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, August 25, 2014

Boniface Wambura azidi kuula TFF

Mkurugenzi Mpya wa Mashindano wa TFF, Boniface Wambura
AFISA Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Boniface Wambura Mgoyo ameula baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mashindano wa shirikisho hilo.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa, Wambura amepandishwa cheo na hivyo ataachana na kiti chake cha sasa cha usemaji wa shirikisho hilo.
Wambura amekuwa kipenzi cha wanahabari kutokana na ushirikiano wake kwa vyomo vya habari na alikuwa katika uongozi uliopita wa rais Leodger Tenga.
Mkurugenzi huyo mpya wa Mashindano wa TFF anatajwa kama Afisa Habari Bora aliyewahi kutokea ndani ya TFF tangu shirikisho hilo lilipobadilisha mfumo wake wa uongozi kwa kuajiri baadhi ya watendaji wake.

No comments:

Post a Comment