STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 8, 2013

Kagera yametemsha kibarua Charles Kilinda

 
MABAO mawili kila moja katika kipindi imeiwezesha klabu ya Kagera Sugar kuzikamata timu za Simba, Mtibwa Sugar na Coastal Union katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kagera ilipata ushindi huo wa mabao 2-0 dhidi ya JKT Ruvu na kusababisha kocha wa maafande hao, Charles Kilinda kutangaza kuachia ngazi kuinoa timu hiyo.
Kagera ilipata ushindi huo katika mechi iliyochezwa jana kenye uwanja wa Chamazi, ambapo bao la kwanza liliwekwa kimiani na Mnigeria, Darlington Ennyima katika dakika ya 33 bao lililodumu hadi mapumziko.
Bao la lililoihakikishia Kagera pointi tatu na kufanye ikifikishe pointi 31 sawa na klabu tatu zilizotajwa hapo juu, liliwekwa kimiani na Juma Nade katika dakika ya 63.
Hata hivyo Kagera imeishia kushika nafasi ya sita nyuma ya Mtibwa Sugar, kwa vile Mtibwa imefunga mabao 22 moja zaidi yao japo uwiano wa mabao ya kufunga wanalingana.

Simba itakayoshuka dimbani Jumapili inaendelea kubaki nafasi ya tatu ikifuatiwa na watakaoumana nao siku hiyo Coastal Union, japo timu hiuzo zinatofautiana mechi walizocheza mpaka sasa.

Msimamo kamili wa Ligi Kuu baada ya mechi ya jana ni:
                             P  W  D  L  GF GA  GD Pts
1 Yanga               18 13  3   2   35  12   23  42
2 Azam                18 11  3   4   31  15  16   36
3 Simba SC          18  8   7   3   26  15  11   31
4 Coastal U          19  8   7   4   21  16   5    31
5 Mtibwa             20  8    7   5   22  18   4   31
6
Kagera Sugar    20  8    7   5   21  17   4   31
7 Ruvu Shooting  18  8    5   5   21  17   4   29
8 JKT Oljoro       19   6   6   7   20  22  -2   24
9 Mgambo JKT    20  7   3   10  14  19  -5  24
10 TZ Prisons      20   4   8   8   11  17  -6   20
11 JKT Ruvu       19   5   4  10  16  30 -14  19
12 Polisi Moro    18   3   6   9   9   18    -9  15
13 Toto African  19   2   8   9  15  27  -12  14
14 African Lyon  20  3   4  13 13  32  -19  13



No comments:

Post a Comment