STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 7, 2013

Barcelona yawatamani Vermaelen, Daniel Agger


VINARA wa Ligi Kuu ya Hispania, Barcelona imetajwa kuwa katika mbio za kuwanasa nyota wa Ligi Kuu ya England, beki wa kati wa Arsenal Thomas Vermaelen na Daniel Agger wa Liverpool kwa ajili ya kuimarisha kikosi chake kilichoanza kupwaya.

Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na the Sun, zinasema kuwa Barca wanamsaka Vermaelen na Agger kwa ajili ya kuziba nafasi ya nahodha wao Carles Puyol ns Eric Abidal ambao umri umeanza kuwatupa mkono ili kuimarisha kikosi chao kushambulia kuanzia nyuma.

Hatua ya Barca kuwafukuzia wakali hao wa EPL imetokana na kukatishwa tamaa na dau kubwa linalotaka mabingwa wa Ujerumani ili kuachia 'kitasa' wao Mats Hummels.

Kwa siku za karibu Barcelona wameonyesha kupoteza ule umahiri wake ambako hivi karibuni katika siku nne walijikuta wakinyanyaswa na wapinzani wao Real Madrid kwa kufungwa jumla ya mabao 5-2 katika mechi mbili.

Walianza kwa kunyukwa mabao 3-1 katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Mfalme kabla ya kulala tena 2-1 katika Ligi Kuu.

Klabu hiyo iliwahi kuingia kwenye mbio za kumwania Agger, 28 kabla ya Manchester City kuingia kati na kusitisha mipango yake na inadhani Vermaelen kwa staili ya uchezaji wake itawasaidia na inamkadiria nyota huyo anaweza kuwa na thamani ya Pauni Milioni 15 na watajaribu kuishawishi Arsenal kuwaachia beki huyo.

No comments:

Post a Comment