STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 7, 2013

Kagera Sugar, JKT Ruvu vitani leo Chamazi

Kikosi cha JKT Ruvu

Kikosi cha Kagera Sugar


BAADA ya kupoteza mechi yake ya mwisho dhidi ya Yanga, timu ya Kagera Sugar jioni ya leo itashuka dimbani kujaribu bahati yake kwa kuumana na maafande wa JKT Ruvu katika mechi ya mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kagera wanaonolewa na nyota wa zamani wa Simba, King Abdallah Kibadeni na Mrange Kabange wakavaana na vijana wa winga wa zamani wa Yanga, Charles Kilinda ambao mechi yao ya mwisho walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Toto Afrika.
Kila upande umejinafasi kufanya vema katika poambano hilo la leo litakjalochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya Dar es Salaam.
Kibadeni alisema kiu yao ni kusaka pointi muhimu ugenini kabla ya kurejea nyumbani kwao Kagera kwa mechi nyingine zijazo.
Kocha huyo alisema kikosi chake kipo tayari kwa pambano hilo na ana imani kubwa ya kupata ushindi licha ya kukiri pambano litakuwa gumu kwa vile JKT Ruvu sio timu ya kubeza hasa ikizingatiwa msimuu huu hawajawa na matokeo ya kuvutia kama misimu miwili iliyopita.
Kwa upande wa JKT Ruvu baadhi ya nyota wake wamedai kama walivyofanya kwa Toto ndiyo itakavyokuwa kwa Kagera katika mechi hiyo kwa nia ya kuipa timu yao ushindi na kuondoka eneo la mkiani wanakochuana na timu nyingine tatu kuwania kuepuka kushuka daraja.
 

No comments:

Post a Comment