STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 7, 2013

Msimbazi kumekucha 'vibopa' wajiuzulu

Zakaria Hanspope (mwenye kofia) na Kaburu (kati) waliotangaza kuachia ngazi Simba leo mchana

HALI ndani ya klabu ya Simba si shwari baada ya vibopa wawili muhimu ndani ya timu Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya utendaji, Zakaria Hanspope na Makamu Mwenyekiti, Godfrey Nyange 'Kaburu' kubwanga manyanga kwa sababu mbalimbali.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana jijini mchana wa leo zinasema kuwa Hanspop amebwaga manyanga kwa kuuandikia barua uongozi wa juu ukitaka kukaa kando kwa kushindwa kutimiza malengo waliyojiweka kutokana na kuwepo kwa mgawanyiko ndani ya uongozi uliopo sasa.
Tayari barua hiyo imeshatua mikononi mwa viongozi wa klabu hiyom unasubiriwa kuridhia maamuzi hayo au la, ikizngatiwa kuwa Hanspop kwa sasa ndiyo kila kitu katika Simba.
Na hivi punde taarifa zimedokeza kuwa Kaburu, ambaye naye ni mmoja wa mhimili wa Msimbazi ameomba kuachia ngazi ikiwa ni katika mtindo ule ule wa kukerwa na hali ya mambo iliyopo ndani ya Simba.
Micharazo imedokeza kuwa, vibopa hao ni mwanzo tu wa kuparaganyika kwa viongozi wa Simba kutokana na kuelezwa kuwa wajumbe kadhaa wa Simba wapo njiani kuwafuata kama njia ya kuonyesha hali si shwari Msimbazi.
Kujiuzulu kwa viongozi hao kunaweza kuwa mwiba kwa Mwenyekiti Ismail Aden Rage ambaye wiki iliyopita alivumishiwa kutaka kuachia ngazi baada ya Simba kulala kwa Mtibwa Sugar katikma mechi ya ligi kuu kabla ya kuibuka na kukanusha taarifa hizo akidai hajiuzulu ng'o kwa vile siyo anayecheza uwanjani.
Simba imekuwa ikifanya vibaya tangu mwishoni mwa duru la kwanza na katika mechi za duru la pili huku wakiwa wameshaaga michuano ya kiimataifa ilipokuwa ikishiriki Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kunyukwa jumla ya mabao 5-0 na Recreativo do libolo ya Angola.


Micharazo inaendelea kuwasaka viongozi wa juu ya Simba kupata undani ya hali ilivyo kadhalika kuwajulisha kinachoendelea, ingawa kinachoonekana Msimbazi sasa ni kuelekea kwenye hali tete huku wakikabiliwa na mechi ngumu siku ya Jumapili dhidi ya Coastal Union na mechi nyingine saba kabla ya kumaliza msimu wa 2012-2013 kukiwa na dalili ya kuutema ubingwa wa ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment