STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 7, 2013

Mtibwa yatakata yazikamata Simba, Coastal Union

Kocha wa Mtibwa, Mecky Mexime

BAO lililofungwa dakika za lala salama kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga, imeiwezesha mabingwa wa zamani wa soika nchini, Mtibwa Sugar kuzikamata timu za Simba na Coastal Union kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mtibwa iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mgambo JKT na kuifanya ifikishe jumla ya poiinti 31 sawa na wapinzani wake hao watakaovaana Jumapili jijini Dar japo wabakia nafasi tano.
Bao hilo pekee la Mtibwa lilifungwa na 'muuaji' wa Simba, Salvatory Ntebe katika dakika ya 90 na kuwafanya vijana wa Mecky Mexime kupumua baada ya kuanza duru la pili vibaya.
Katika mechi nyingine zilizochezwa jana kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid wenyeji JKT Oljoro iliibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa katika kipindi cha pili na Paul Nonga na kuilaza Prisons ya Mbeya ambapo kocha wake Jumanne Chale alilalamikia mchezo huo.
Kocha huyo alidai wenyeji walibebwa kutokana na kukataliwa bao lao safi lililofungwa na mchezaji wake, huku akidai kulikuwa na maamuzi yasiyomvutia kwenye pambano hilo.
Nao maafande wa Ruvu Shooting ya Pwani waliendelea kuizamisha Aficna Lyon kwa kuilaza baio 1-0 na kuifanya timu hiyo kubakia mkiani mwa msimamo wa lihi hiyo itakayoendelea tena leo.
Bao lililoiweka pabaya Lyon katika kuwepo kwake katika Ligi Kuu msimu ujao lilifungwa na Abdulrahman Mussa katika dakika ya 29 katika mechi kali iliyochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, jijini Dar.

No comments:

Post a Comment