STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 21, 2015

Barcelona yazamishwa nyumbani na Malaga

Barcelona 0-1t Bat BA Malaga
Juanmi akiitungua Barcelona leo
Barcelona forward Lionel Messi (left) vies with Malaga's forward Samuel Castillejo (right) on Saturday
Messi hakufua dafu leo kwa Malaga siku chache kabla ya Barcelona kuvaana na Manchester City kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
KLABU ya Barcelona ikiwa dimba la nyumbani la Camp Nou imekubali kipigo cha bao 1-0 mbele ya Malaga katika mfululizo wa Ligi ya Hispania, La Liga.
Kipigo hicho cha nne kwa Barcelona msimu huu katika ligi hiyo kimezidi kuongeza ushindani wa mbio za ubingwa dhidi ya watetezi Real Madrid ambayo watashuka dimbani kesho wakiwa ugenini.
Bao pekee la wageni Malaga mbele ya Barcelona liliwekwa kimiani na  Juanmi katika dakika ya saba ya mchezo huo na kungángánia hadi mwisho na kuwaacha Barcelona wakiwa hoi nyumbani.
Mechi nyingine inayochezwa hivi sasa Valencia wakiwa ugenini waongoza bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Cardoba.

No comments:

Post a Comment