STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 10, 2013

Mesut Ozil akandia Real Madrid

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg4ofh6d-gXibmGvc2xSsD8UfdtNJEaoqFh5VR-k8V5ZtbFQkA38OgBh_eW2UhZjNmxZJun5lUreGf6kmv9B3JxAoWcDyI6DqafsqZSqnXRzd4hrsJsA7mPvEmI-S1M0stt-cf073BC4981/s640/Mesut+Ozil+2013_1.jpg
MESUT Ozil amedai kwamba angejiunga Arsenal hata bure  na amebainisha kwamba "uwazi, kuaminiwa na kuheshimiwa" vilipotea Real Madrid.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani alikamilisha uhamisho wake wa siku ya mwisho ya usajili na kutua katika kikosi cha Arsene Wenger kwa dau la uhamisho la paundi milioni 40, akisaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo.
Ozil alibainisha kuwa mazungumzo na kocha huyo wa Arsenal yalimshawishi kupima hali yake ndani ya Real Madrid na kumvutia kuhamia kwenye Ligi Kuu ya England.
“Kwa namna fulani, mazungumzo yale yalinivutia kuhama na kunifanya nitambue kuwa nilichokipoteza Madrid: uwazi, kuaminiwa, kuheshimiwa," Ozil aliliambia gazeti la Die Welt.
"Yeye (Wenger) aliniambia vile anavyoniona, namna anavyonihitaji, na kile anachotarajia kutoka kwangu.
"Siwezi kufanya chochote kuhusu ada ya uhamisho. Ningeweza kuja hata bure."
Ozil, mchezaji aliyenunuliwa kwa ada iliyovunja rekodi ya uhamisho kwa Arsenal, alifunga ama kutoa pasi za magoli 108 katika mechi 159 katika michuano yote akiwa na Madrid.

No comments:

Post a Comment