STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 15, 2011

BOB JUNIOR AMCHAMBUA DIAMOND



MWIMBAJI na mtayarishaji wa muziki wa Bongo Fleva kutoka kundi la ‘Masharobaro’, Bob Junior ‘Rais wa Masharobaro amesema kuwa sababu ya msanii, Nasib Abdul ‘Diamond’ kukosa tuzo mwaka huu inasababishwa na kujikweza kwake.
Alisema Dimond baada ya kupata tuzo tatu mwaka jana amekuwa anajisikia na kujiona huku akitafuta wanawake wenye sifa mbaya ili aweze kuandikwa.
Bob Junior ambaye ndiye alitayarisha albamu ya msanii huyo ya kwanza alisema kuwa sifa zinamfanya msanii huyo kushindwa kufanikiwa katika tuzo za mwaka huu.
“Msanii huyo amekuwa akinitafuta hata mimi na kufikia kunilalamikia kuwa namuongezea fedha za kutengenezea nyimbo, kitu ambacho ni maamuzi ya kiofisi.
Alisema kuwa ukiachilia suala la kuchukua jina lake la Rais wa wasafi akibadilisha jina lake la rais wa masharobaro ambalo lina maana hiyo kwa sasa amekusanya genge kwa nia ya kumfanyia kitu kibaya, hali iliyomfanya atoe taarifa kituo cha polisi
http://mamapipiro.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment