STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 15, 2011

Ligi ya Kick Boxing sasa Juni





MICHUANO ya Ligi ya Ubingwa kwa Mchezo wa Kick Boxing iliyokuwa ichezwe mwishoni mwa Machi, imesogezwa mbele hadi Juni mwaka huu.
Mratibu wa michuano hiyo, Japhet Kaseba, alisema ligi hiyo imekwama kufanyika kutokana na kutingwa na mazoezi ya maandalizi ya pambano lake la Ngumi za Kulipwa kati yake na bondia Mada Maugo.
Kaseba atapigana na Maugo, wiki ijayo kwenye ukumbi wa PTA, Dar es Salaam katika pambano lisilo na mkanda la uzito wa kilo 72 kuwania nafasi ya kupigana na bingwa wa dunia, Francis Cheka wa Morogoro.
Akizungumza na MICHARAZO, Kaseba, alisema kubanwa na mazoezi kumemfanya ashindwe kuratibu ligi hiyo na kusema, mara baada ya pambano lake atatangaza tarehe rasmi ya ligi hiyo ingawa alisema kuna uwezekano ikafanyika mwezi Juni.
"Nimeshindwa kuratibu ligi kama nilivyopanga ifanyike Machi na sasa natarajia ifanyike Juni, ingawa tarehe nitaitangaza baada ya kumaliza pambano langu dhidi ya Maugo ambalo ndilo lililonifanya niwe 'bize', nataka kumpiga nikapigane na Cheka," alisema.
Kuhusu maandalizi ya pambano hilo, Kaseba alisema anaendelea vema na ana matumaini makubwa ya kushinda pambano hilo, la raundi 10 lililoandaliwa na Double K Entertainment, litakalosimamiwa na TPBO inayoongoza na Rais wake, Yasin 'Ustaadh' Abdalla.
"Kwa kweli naendelea vema, najifua usiku na mchana kuhakikisha nakuwa fiti nimpige Maugo, ili nikavaane na Cheka kuthibitishia mashabiki wangu kuwa, sikupigwa kihalali na Cheka kwenye pambano letu la uwanja wa Uhuru," alisema Kaseba.


Mwisho

No comments:

Post a Comment