STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 15, 2011

Wakazi wa Udzungwa kufunzwa namna ya kutunza Mbega

SHIRIKA lisilo la kiserikali la STR8 UP Vibes imeandaa warsha maalum kwa wakazi wanaoizunguka hifadhi ya Udzungwa juu ya kuwatunza wanyama aina ya Mbega wekundu wanaopatikana kwenye hifadhi hiyo.
Warsha hiyo imepangwa kufanyika hivi karibuni, mkoani Morogoro, ambapo mbali ya kuwatunza wanyama hao lakini pia itakuwa na lengo la kutoa elimu ya kuvitunza vyanzo vya maji.
Akizungumza na Mtandao huu, mratibu wa warsha hiyo, Salum Kondo alisema kuwa, wameamua kuandaa warsha hiyo ili kuwapa elimu ya kutosha watu wote wanaoishi kando kando ya hifadhi za taifa kujua jinsi ya kuwatunza wanyama na vyanzo vya maji.
Kondo, alieleza kuwa kwa kuanzia wamemua kuanza na mkoa wa Morogoro, ambapo baadaye wataaendelea kwenye mikoa mingine iliyo na hifadhi za Taifa.
"Dhumuni letu ni kuwapa elimu watu wote wanaishi karibu na hifadhi za Taifa, lakini kutokana na umuhimu wa hifadhi za Udzungwa, tumekubaliana tuanzie huko" alisema.
Aliongeza kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa la kuwauwa Mbega Wekundu, hali ambayo inaweza kusababisha wanyama hao kutoweka kabisa Duniani.
Kondo aliongeza kuwa kwa kuwa wanyama hao hupatikana, Udzungwa pekee, wameona kuna haja ya kuwalinda kwa gharama yeyote.
"Kama wakazi wa wanaizunguka hiafdhi ya Udzungwa watapatiwa elimu ya kutosha juu ya kuwatunza wanyama hao na namna ya kuwatumia kuwaingizia kipato, bila shaka wataacha kuwaua," alisema.
Kondo alisema katika Kongamano hilo litakalofanyika mkoani Morogoro linatarajia kuwashirikisha wadau mbali ikiwa ni pamoja na wanavijiji, wataalam kutoka wizara ya Maliasili na Utalii, ambapo pia kutakuwa na burudani mbalimbali zitakazowakilisha mila na tamaduni za mkoa huo.

No comments:

Post a Comment