STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 15, 2011

Tundaman ni Bora Tuachane tu



MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya toka kundi la Tip Top Connection, Khaleed Ramadhan 'Tundaman', ameachia kibao kipya kiitwacho 'Bora Tuachane', akiwa mbioni kufyatua wimbo mwingine akiwashirikisha Mapacha wa kundi la P Square la Nigeria.
Nyimbo hizo mbili ni maandalizi ya kufyatuliwa kwa albamu yake mpya itakayokuwa ya nne kwa msanii huyo aliyetumbukia kwenye sanaa ya muziki mwaka 2007 akitokea kwenye soka.
Akizungumza na MICHARAZO, Tundaman, alisema kibao hicho cha 'Bora Tuachane' ambacho kinatarajiwa kusambazwa hivi karibuni ni simulizi la kweli linalomhusu yeye.
"Wakati albamu yangu ya Hali Yangu Mbaya ikitamba sokoni, nimeanza maandalizi ya kufyatua albamu mpya ya nne, ambapo nimeachia ngoma inakwenda kwa jina la 'Bora Tuachane' ambao ni simulizi la kweli linalonihusu mimi mwenyewe," alisema Tundaman.
Msanii huyo, mwenye mtoto mmoja wa kike aitwae Khairat, alisema kama zilivyo nyimbo zake za nyuma, kibao hicho kipo katika mahadhi ya 'kulalamika' na kutamba kitabamba kutokana na ujumbe uliopo na midundo yake inayovutia.
Aliongeza mbali na kibao hicho, pia ana wimbo mwingine mpya ambao ataimba kwa kushirikiana na wasanii wawili mapacha wa Nigeria, P Square.
"Kibao kingine ninachokiandaa ni The All One, ambacho nimewatumia mistari P Square ili waweke sauti zao, kabla ya kuja kuchanganywa, mie nitaimba kiswahili na wao wataimba kwa lugha ya Kiingereza, lengo likiwa ni kusaka hadhi ya kimataifa," alisema.
Tundaman, aliyewahi kuzichezea timu za Friends Rangers na Yanga kabla ya kuhamia kwenye muziki, hadi sasa ana albamu tatu, ambazo ni Neila iliyomtambulisha rasmi kwenye ulimwengu wa muziki huo, Nipe Ripoti alioshirikiana na Spark na Hali Yangu Mbaya, aliyoachia hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment