STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 15, 2011

Mafisango ambadili Humud Simba






KIUNGO aliyetua Msimbazi kwa mbwembwe na kuishia kushindwa kutamba katika timu ya Simba kutokana na majeruhi ya mara kwa mara, Abdulhalim Humoud, ametua Azam akipishana na beki Mnyarwanda Patrick Mafisango.
Humoud aliyesajiliwa na Simba msimu uliopita akitokea Mtibwa Sugar, ikiwa ni siku chache tangu ang'are kwenye pambano la kihistoria la kimataifa kati ya Tanzania na Brazil, ni miongoni mwa wachezaji wapya waliotua Azam kwa ajili ya msimu ujao.
Kwa mujibu wa taarifa za mtandao wa klabu hiyo, kiungo huyo anayependa kufananishwa na Ronaldinho Gaucho, ametua Azam akibadilishana na beki Mafisango aliyeenda Msimbazi kuimarisha kikosi chao kilichopoteza ubingwa kwa Yanga.
Wachezaji wengine wapya waliotuma Azam, ikiwa ni kati ya wachezaji 20 waliopendekezwa na kocha wao, Stewart Hall ni pamoja na aliyekuwa kipa wa Yanga,
Obren Cuckovic toka Serbia na Mwadini Ally aliyekuwa Mafunzo ya Zanzibar.
Pia wamo Waziri Salum toka Mafunzo, Ghulam Abdallah wa Chuoni Zanzibar, Zahor Pazi wa African Lyon na nyota wa Ocean View, Khamis Mcha 'Viali'.
Habari hizo zinasema kuwa hao ni sehemu ya wachezaji wapya wanaotua Azam kuungana na wachezaji wengine walioisaidia klabu hiyo kushika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambao wameshasainishwa mikataba mipya.
Wachezaji hao kwa mujibu wa mtandao huo ni Manahodha Ibrahim Shikanda na Aggrey Moris, Malika Ndeule, Lackson Kakolaki, Erasto Nyoni, Ibrahim Mwaipopo, Seleman Kasim Selembe, Kalimangonga Ongala, Jamal Mnyate, Mrisho Ngassa na John Bocco.
Wachezaji vijana waliokuwa wamepandishwa kwenye kikosi hicho toka timu ya vijana na kubakishwa ni Himid Mao, Salum Aboubakar na Jamal Mnyate, wakiongezewa nguvu na kipa Daudi Mwasongwe aliyepandishwa toka Azam Academy.
Makipa Vladmir Nhyonkulu na Jackson Chove pamoja na wachezaji wengine kama saba walioichezea timu hiyo wapo katika hatihati ya kuendelea kubaki katika kikosi hicho kinachosukwa kwa ajili ya kuongeza upinzani kwa msimu ujao wa ligi kuu nchini.

Mwisho

No comments:

Post a Comment