STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 15, 2011

Madee kudondosha nyingine



MSANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya nchini, Hamad Ally 'Madee', anatarajia kuachia hewani ngoma nyingine mpya baada ya wiki mbili zilizopita 'kudondosha' audio na video ya kibao kipya cha 'Napeleka Benki'.
Ingawa Madee hakuweza kuweka bayana kibao kipi kitakachofuata baada ya 'Napeleka Benki', lakini alisema wiki ijayo ataachia kazi nyingine mpya wakati akiendelea na maandalizi ya kupakua albamu yake mpya na ya nne.
Kiongozi huyo wa kundi la Tip Top Connection, alisema moja kati ya nyimbo zake saba alizokamilisha itaachiwa kuzidi kuitambulisha albamu hiyo mpya itakayokuwa na nyimbo nane.
"Natarajia kuachia wimbo mwingine mpya baada ya 'Napeleka Benki', sijui itakuwa ipi kati ya 'Nisikilize', 'Siku ya Mwisho', 'Mtasubiri', 'Pendo', 'Hifla', 'Amka' au 'Siri Zote Ninazo Mimi'," alisema Madee.
Madee alisema nyimbo zote za albamu hiyo ya nne tangu alipoingia kwenye fani ya muziki zimerekodiwa katika studio mbili tofauti za MJ Production na Bongo Records chini ya watayarishaji Makochali, Master J na P Funk.
Ingawa bado hajaipa jina albamu yake ijayo iitwe vipi, lakini hiyo itakuwa ni albamu ya nne kwa Madee baada ya awali kutamba na 'Kazi ya Mola', 'Hip Hop Haiuzi' na 'Pesa'.Msanii huyo aliyesherehekea siku yake ya kuzaliwa mwanzoni mwa wiki hii, aliwahi kutangaza kutaka kustaafu muziki, ili apumzike na kujiendeleza kimasomo, lakini kwa ushauri wa watu wake wa karibu pamoja na mashabiki wa muziki aliamua kufuta wazo hilo lililokuwa alifanye mwaka juzi.

No comments:

Post a Comment