STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 15, 2011

Mbio za usajili zaanza Bara * Mastaa wa vigogo matumbo joto * Zilizopanda zawanyemelea







PAZIA la usajili wa wachezaji kwa timu za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa ajili ya msimu ujao wa limefunguka kwa klabu mbalimbali kupigana vikumbo kupata saini za nyota inayowahitaji.
Ingawa, Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, halijatangaza zoezi ya usajili litaanza lini, tayari vilabu kadhaa vimeshaanza kujinadi kuwanasa wachezaji wapya na kuwafungulia milango ya kutoka wasiowahitaji kwa msimu ujao, huku Simba, Yanga na Azam zikiongoza kwenye mbio hizo.
Simba ambayo ilipoteza ubingwa kama utani kwa watani zao, imedaiwa imeshawatangazia baadhi ya wachezaji wake kuwa waangalie ustaarabu wake, huku ikiwa imeshawasainisha wachezaji kama Mwinyi Kazimoto toka JKT Ruvu, Patrick Mafisango na wengine wakiendelea kuwafukuzia.
Walioachiwa milango ya kutokea hadi sasa, ingawa haijatangazwa rasmi ni pamoja na kipa Juma Kaseja, kiungo Mohammed Banka, Mussa Hassani Mgosi, Joseph Owino, Hillary Echessa, Salum Kanoni, Anthony Matangalu, Mohammed Kijuso na David Naftal waliokuwa kwa mkopoa klabu za AFC Arusha na Majimaji Songea.
Pia katima orodha hiyo anatajwa beki Kelvin Yondan, ambaye inadaiwa yu mbioni kutua kwa mahasimu wa Simba, Yanga iliyokuwa ikimwinda kwa muda mrefu.
Inaelezwa Yanga inamtaka Kelvin kutokana na kuwepo kwa taarifa kwamba beki wake, Nadir Haroub 'Cannavaro' yu mbioni kutua Azam iliyoanza kumnyemelea tangu msimu ulioisha karibuni.
Yanga wenyewe tayari imeshawapoteza wachezaji wao wawili 'mapro', Mghana Ernest Boakye na Ivan Knezevic wanaodaiwa watakipiga msimu ujao ndani ya Azam Fc.
Ingawa, Yanga imesema inasubiri mapendekezo ya kocha wake, Sam Timbe kuimarisha kikosi chao, baadhi ya wachezaji wanaodaiwa hawatakuwa na timu hiyo msimu ujao ni pamoja na Issac Boakye wa Ghana, Nsa Job, Shamte Ally, Nelson Kimath na wengine walioonekana kuwa 'mizigo'.
Baadhi ya klabu zilizopanda daraja msimu huu zenyewe zinatajwa kuwavizia baadhi ya nyota watakaoachwa katika klabu hizo kubwa ili kuimarisha vikosi vyao kabla ya kushiriki ligi hiyo ngumu na kubwa kwa Tanzania.
Timu zilizopanda daraja toka Ligi Daraja la Kwanza ni pamoja na Villa Squad na Moro United za Dar, JKT Oljoro ya Arusha na Coastal Union ya Tanga inayorejea tena kwenye ligi hiyo.

No comments:

Post a Comment