STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, April 15, 2011

Ray kumbe ni 'Handsome wa Kijiji'

WAKATI filamu yake ya 'Second Wife' ikiendelea kutesa mitaani kwa sasa, msanii mkali wa filamu nchini, Vincent Kigosi 'Ray' amekamilisha kazi yake nyingine mpya iitwayo 'Handsome wa Kijiji', ambayo kwa mara ya kwanza ameigiza kama mtu dhalili aishie kijijini tofauti na alivyozoeleka.
Filamu hiyo iliyokamilika wiki iliyopita imerekodiwa maeneo ya Bagamoyo, mkoani Pwani, baada ya ushauri wa mashabiki wake waliodai wamechoshwa kila mara kumuoa akiigiza kama mtu tajiri anayeishia kifahari mjini, na hivyo kumlazimisha kutekeleza wazo hilo na kwenda 'bush'.
Kazi hiyo mpya ambayo imewashirikisha wakali kadhaa wa fani hiyo nchini kama Ben Blanco, Mzee Magali, Tash, Hashim Kambi, Irene Paul na wengine ipo kwenye uhariri tayari kupelekewa sokoni.
Katima ujumbe kwa mashabiki wake, Ray, amewataka amewataka wadau wa filamu kukaa mkao wa kula kushuhudia picha ya aina yake ambayo, ndani yake ameigiza kwa jina la Hamza.
"Wadau wa kiwanda cha filamu Tanzania napenda kuwafahamisha kuwa filamu yenu mpya ya kipekee na yenye manjonjo mengi sasa yakamilika," sehemu ya ujumbe wa Ray kupitia mtandao wake unasomeka hivyo.
Pia unaongeza; Nawashukuru sana kwa kuweza kufuatilia mchakato mzima wa sinema yenu ya Handsome wa Kijiji subirini sana wadau mzigo huu maana kampuni ya Rj Company imekuja tofauti kabisa na watu walivyozoea."
Filamu hiyo ni ya tatu kwa Ray ndani ya mwaka huu, baada ya awali kuachia 'Family Disaster' na kisha 'Second Wife' iliyopo sokoni kwa sasa ikiendelea kufanya vema kati ya kazi zilizotoka mwezi uliopita.

No comments:

Post a Comment