STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 12, 2011

Kanumba atambia 'The Shock'



MUIGIZAJI Nyota wa Filamu Tanzania, Steven Kanumba, ametamba kuwa kazi yake mpya ya 'The Shock' ambayo ipo kwenye foleni kabla ya kuachiwa mitaani ni 'funika bovu' ya mwaka 2011.
Kanumba, mshindi wa tuzo ya Muigizaji Bora wa Kiume 2010, alisema filamu hiyo iliyoandaliwa na kampuni yake ya Kanumba The Great Films ni moja ya kazi itakayokimbiza kwenye soko la filamu kutokana na namna iliyoandaliwa pamoja na washiriki wake walivyofanya kweli.
Akizungumza na Micharazo, Kanumba, alisema sio kawaida yake kujisifu, ila kazi hiyo ni moja ya kazi nzuri iliyouanza mwaka 2011.
Alisema wakati kazi hiyo ambayo inamuibua muigizaji mpya wa kike nchini Shez Sadry, ikiwa kwenye foleni kabla ya kuingia mitaani, kampuni yake inaendelea na maandalizi ya kazi nyingine.
"Sio siri kama kuna kazi itakayokimbiza mwaka huu, basi ni The Shock, kutokana na jinsi nilivyoiandaa na namna washiriki walivyofanya kazi ya ziada kudhihirisha kuwa fani yetu inazidi kupaa nchini," alisema.
Washiriki wengine waliopo ndani ya filamu hiyo ni mwanamuziki mahiri wa bendi ya FM Academia, Patcho Mwamba na wengine wengi.
Katika hatua nyingine, kampuni ya kusambaza filamu ya Kapico, imeamua kuibeba filamu mpya ya kusisimua ya Bangkok Deal inayohusisha majoka makubwa kama ilivyokuwa 'Anaconda'.
Filamu hiyo iliyoandaliwa na kampuni ya Huba Production, imewashirikisha wasanii wakali kama Charles Magali, Bambucha na wengine, wakati wowote itakuwa hewani kupitia Kapico moja ya wasambazaji wakubwa wa filamua za Kibongo nchini.
Mwisho

No comments:

Post a Comment