STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 12, 2011

Benita: Kimwana aliyekacha 'utawa' aigize







TAMTHILIA ya 'Beyond Our Dreams'iliyokuwa ikirushwa kupitia kituo cha runinga cha NTA miaka ya katikati ya 1996 ndiyo iliyomtangaza Benita Nzeribe, mmoja wa waigizaji nyota wa Nigeria.
Mwaka 1998 alijitumbukiza kwenye fani ya uchezaji filamu na kazi mbili za awali za 'Notorious Virgin' na 'Gold Diggers' zilizomtangaza vema kwenye ulingwengu wa fani hiyo.
Filamu hizo ilitoka mwaka 1999-2000 na tangu hapo ameshiriki kazi mbalimbali zilizomjengea jina katika ukanda wa Nollywood na kufahamika kimataifa.
Mzaliwa huyo wa Jimbo la Anambra aliyewahi kunusurika kufa kwenye ajali ya gari, alisema pamoja na kipaji cha sanaa kuwa cha kuzaliwa, lakini kuvutiwa kwake na waigizaji Liz Benson wa Nigeria, Angeline Jolie na Cameroon Diaz wa Marekani ndiko kulikomtumbukiza huko.
Alisema, hata alipojiunga na Chuo Kikuu cha Abia, lengo lake lilikuwa kusomea masomo ya sanaa, lakini chuo hicho hakikuwa na kozi hizo na hivyo kuchukua masomo ya Lugha ya Kiingereza aliyohitimu kabla ya kuanza kuuza sura kwenye runinga.
Aliongeza kuwa bahati nzuri ni kwamba alipoanza kuigiza wazazi wake hawakumuangusha, ingawa baadhi ya wahitimu wenzake walimshangaa kwa kuichagua kazi hiyo ya uigizaji.
Benita, mtoto wa tatu kati ya wanne wa mfanyabiashara maarufu Mr Nzeribe na mama muuguzi mstaafu, tangu alipoanza kushiriki uigizaji wa filamu amecheza zaidi ya kazi 100 kati ya hizo akishirikiana na wakali kama mkongwe Olu Jacobs, Ejike Asiegbu, Ken Okonkwo, Fred Amata, Juliet Ibe na wengineo.
Moja ya filamu anayojivunia ni ile ya Peace of Mind, aliyocheza kama mke anayenyanyaswa na kupigwa na mumewe, kitu alichodai kimewahi kumtokea katika maisha yake ya kimapenzi.
Mwanadada huyo, ambaye pia ni mwanamitindo na mpambaji, majina yake kamili ni Benita Nnenna Adaeze Nzeribe, aliyezaliwa Uzoakwa, Ihiala, Jimbo la Anambra, elimu yake ya msingi na sekondari aliisoma katika miji ya Aba na Umuahia.
Pia alipitia mafunzo ya kiroho akiwa na lengfo la kuja kuwa mtawa, kabla ya kufuta wazo hilo na kati ya vitu anavyokumbuka katika makuzi yake ni tukio la baba yake kumnunulia gari lake la kwanza akiwa na miaka 14 tu.
"Tukio hili la baba kuninunulia gari nikiwa na miaka 14 siwezi kulisahau maishani mwangu kwani lililonyesha alivyonijali na kunithamini," alinukuliwa.
Kuhusu uigizaji wake wa filamu za kimapenzi, alisema ni jambo la kawaida kulingana na nafasia anayopangiwa na muongozaji wake, ila ni mtu anayejiheshimu na kuithamini kazi yake.
Alipoulizwa kama yupo tayari kuchojoa ili aigize utupu, Benita alisema katu hawezi kufanya upuuzi huo hata kwa kisi gani cha fedha hasa kutokana na hadhi ya familia yake nchini kwao.
Baadhi ya kazi alizoshiriki kisura huyo, mbali na zile zilizomtambulisha Nollywood ni Cross My Heart, Cross & Tinapa,Endless Madness,Tears of a Saint, Treasure Hunt,Breath Again,Buried Emotion,Enemies in Love, Games Men Play, Girls Cot,King of the Town na Life Abroad.
Pia ameshiriki Peace Talk, The Final Days, Christian Girls, Fools in Love, Hold Me Down, Paradise to Hell, Secret Affairs, The Scorpion, Under Arrest, Beyond Reason, My Desire,Stand by Me, A Night to Remember, Arrows, Great Change, Lagos Babes, Mission to Africa, Saved by Grace, Street Life, The One I Trust, Agony of a Mother, Fire on the Mountain na kadhalika.

No comments:

Post a Comment