STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 12, 2011

Sikinde wavamia ngome ya Msondo

BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Mlimani Park 'Sikinde' imevamia ngome ya wapinzani wao, Msondo Ngoma kwa kuanzisha bonanza linalofanyika kila Jumapili kwenye ukumbi wa TCC Club-Chang'ombe.
Msondo kwa muda mrefu imekuwa ikifanya bonanza kila Jumamosi kwenye klabu hiyo, hivyo kutua kwa Sikinde ni kama kuwachokoza ikiwa ni wiki kadhaa tangu pambano lao kuahirishwa.
Katibu wa bendi ya Sikinde, Hamis Milambo, alisema bendi yao imelianza bonanza hilo tangu wiki iliyopita kwa kutumbuiza kuanzia saa 8 mchana hadi saa 12 kabla ya kumalizia burudani zao kwenye ukumbi wa SUWATA.
Milambo, alisema hilo ni bonanza la pili kwa bendi yao, baada ya kufanya pia bonanza jingine linalifahamika kama Konyagi Bonanza kila Jumamosi kwenye ukumbi wa DDC Kariakoo.
"Tangu wiki iliyopita tumekuwa tukifanya bonanza jipya kwenye ukumbi wa TCC Chang'ombe majira ya saa 8-12 kisha kuendelea na ratiba yetu pale SUWATA kuanzia saa 1-5 usiku," alisema.
Aliongeza kwa leo bendi yao itakamua kwenye bonanza lao la Konyagi ikitambulisha nyimbo zao mpya na zile za zamani zilizoifanya bendi hiyo kuwa Mabingwa wa Muziki Tanzania.
Baadhi ya nyimbo mpya za bendi hiyo ni Tunu ya Huba, Wanawake Wakiwezeshwa, Urithi, sambamba na zile za albamu yao ya Supu Imetiwa Nazi.
Mwisho

No comments:

Post a Comment