STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 12, 2011

Filamu ya ngumi hadharani leo



FILAMU mpya inayozungumzia maisha ya bondia wa zamani na kocha wa sasa wa klabu ya Ashanti, Rajabu Mhamila 'Super D' iitwayo 'Super D:Boxing Coach', inatarajiwa kutolewa rasmi leo.
Filamu hiyo ambayo inahusisha pia mapambano kadhaa ya mabondia nyota duniani, itatolewa rasmi leo katika sherehe maalum itakayofanyika kwenye klabu ya ngumi ya Ashanti inayoadhimisha mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake.
Akizungumza na micharazao, Super D, aliyewahi kuzichezea klabu za Simba, Reli na Amana na kupigana na mabondia kama Mbwana Ally na wengineo, alisema filamu hiyo ni maalum kwa ajili ya kuhamasisha mchezo wa ngumi ambao umeshuka kiwango kwa sasa.
"Pamoja na kusimulia na kuonyesha michezo yangu tangu wakati nikipigana mwaka 1984, pia kuna mapambano ya wakali wa dunia katika mchezo wa ngumi za kulipwa," alisema Super D.
Super D, alisema filamu hiyo itazinduliwa leo na kuachiwa hadharani ili mashabiki wa ngumi na filamu kwa ujumla kuipata na kwenda kuishuhudia uhondo wake.
Aliyataja mapambano yaliyopo ndani ya filamu hiyo kuwa ni, ya Muhammad Ally, Iron Mike Tyson, Manu Pacquiao, Michael Moore, Llyod Mayweather, Oscar de La Hoya na wengineo.
"Kazi yangu itakuwa mitaani kuanzia Machi 12, wakati tukiadhimisha mwaka mmoja tangu Ashanti Boxing ianzishwe mie nikiwa miongoni mwa makocha wake," alisema.
Hiyo itakuwa ni filamu ya pili inayozungumzia mabondia wa zamani na mafunzo ya ngumi, awali bingwa wa dunia, Francis Cheka 'SMG' akifanya hivyo mwaka juzi kwa kutoa filamu kama hiyo ikiwa na jina na Francis Cheka na Historia Yake.

No comments:

Post a Comment