STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 25, 2011

Stone Mayiyasika wanasa watano

BENDI ya Stone Mayiyasika 'Vijana wa Kazi' imeimarisha safu ya ushambuliaji wa jukwaa kwa kunasa wanenguaji watano akiwemo mnenguaji mahiri aliyewahi kutamba na bendi ya Twanga Pepeta, Juma Mohamed (Super Danger).
Mratibu wa bendi hiyo, Pascal Mahollelo, alisema wanenguaji hao watano wameanza mazoezi na katika maonyesho yao yote ya kusheherekea sikukuu ya Pasaka wataanza kuwatambulisha kwa mashabiki.
Alisema, mbali ya Super Danger ambaye ni mkongwe, wanenguaji wengine wapya ni wa kike na kwamba ni chipukizi ambao wameonyesha uwezo mkubwa wa kazi.
Aliwataja wanenguaji hao wa kike kuwa ni Zawadi Seif, Joselina Ngatunga (Happy), Shania Malimba na Mwanahamisi Ramadhan.
"Sisi hatuhitaji kugombana na watu ndiyo maana tumeona tuwatengeneze wetu wenyewe na nina imani mashabiki watawakubali kutokana na umahiri wao jukwaani" , alisema Mahollelo.
Alisema, utambulisho wa wanenguaji hao ungeanza kwenye maonyesho yao Sikukuu ya Pasaka.

No comments:

Post a Comment