STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 25, 2011

Sikinde wana mbili mpya



BENDI ya Mlimani Park 'Sikinde' imekamilisha vibao viwili ikiwa ni moja ya mikakati yake ya kujipanga upya baada ya kuondokewa na mwanamuziki wake, Shaaban Dede aliyejiunga na mahasimu wao, Msondo Ngoma.
Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo, alisema kuwa bendi yao ambayo kwa wiki mbili mfululizo imekuwa kambini ikijifua, ambapo imekamilisha nyimbo mbili zilizotungwa na muimbaji wao mkongwe, Hassani Bitchuka.
"Tumeanza kujipanga upya kwa ajili ya kupakua albamu mpya na tayari tupo kambini kwa wiki ya pili sasa, ambapo tumeshakamilisha nyimbo mbili mpya zilizotungwa na Bitchuka," alisema.
Katibu huyo alisema nyimbo hizo zinazoendelea kufanyiwa mazoezi, hazijapewa majina hadi sasa na zitatambulishwa kwa mashabiki wao katika maonyesho yao ya Sikukuu ya Pasaka.
"Tutazitambulisha kwenye maonyesho yetu ya Pasaka, na hapo ndipo zitakapofahamika majina yake, ila ni kati ya nyimbo zitakazothibitisha kuwa Sikinde ni mabingwa wa muziki wa dansi nchini," alisema Milambo.
Milambo alisema baada ya maonyesho ya Pasaka, bendi yao itarejea kambini kwa ajili ya kumalizia kuzifanyia mazoezi nyimbo nyingine mpya ambazo zimeshaandikwa mashairi na waimbaji wao, Abdallah Hemba na Hassani Kunyata tayari kukamilisha idadiu ya nyimbo zinazotakiwa kwa albamu yao ijayo.
Tangu mwaka juzi, Sikinde ilipotoa albamu yao ya Supu Imetiwa Nazi, bendi hiyo haijaachia albamu nyingine zaidi ya vibao viwili vya Wanawake Wanaweza na Tunu ya Upendo vilivyotungwa na Dede maarufu kwa sasa kama 'Mzee wa Loliondo' ambaye ameenda Msondo Ngoma.

No comments:

Post a Comment