STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 25, 2011

Tamasha la ngumi laanzishwa Dar

MABONDIA mbalimbali wakiwemo wakongwe na chipukizi wanatarajia kujumuika pamoja katika tamasha maalum la ngumi linaloanza rasmi kesho kwenye Manispaa ya Ilala, jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Kinyogoli Foundation inayomilikiwa na bondia wa kimataifa wa zamani ambaye ni kocha kwa sasa, Habib Kinyogoli, awali lilipangwa kufanyika leo Jumatatu ya Pasaka, kwenye ukumbi wa Panandipanandi.
Akizungumza na MICHARAZO, mmoja wa waratibu wa tamasha hilo, Rajabu Mhamila 'Super D' alisema katika tamasha hilo, mabondia mbalimbali wakongwe na chipukizi watachuana na lengo ni kuwapa nafasi chipukizi ya kujifunza mbinu kutoka kwa mabondia hao wazoefu.
Super D ambaye pia ni bondia wa zamani na kocha wa klabu ya Ashanti, alisema yeye na Kinyogoli, wameamua kushirikiana kuandaa tamasha hilo ili kuhakikisha mchezo wa ngumi nchini unarejesha heshima yake baada ya kudorora kwa muda mrefu.
"Katika kurejesha hadhi ya ngumi nchini, tumeamua kuandaa tamasha la ngumi ambalo litakuwa likifanyika kila wiki kwenye ukumbi wa Panandi Panandi ambapo wakongwe na mabondia wanachipukia watashirikiana kupigana katika kutoa burudani," alisema Super D.
Aliongeza kuwa, mbali na michezo kadhaa ya ngumi, ikiwahusisha baadhi ya nyota wa mchezo huo kama mabondia wa ukoo wa Matumla, pia tamasha hilo litapambwa na burudani kemkem za muziki kutoka kwa wasanii ambao watakakuwa wakipokeza kwenda kutumbuiza kama njia ya kuwahamasisha watu kuhudhuria kwa wingi.

No comments:

Post a Comment