STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, July 9, 2011

Klabu za ngumi kupepetana Ilala

KLABU za ngumi za ridhaa za Amana na Matimbwa ni miongoni mwa klabu zaidi ya tano zinazotarajiwa kuonyeshana kazi katika mfululizo wa michuano maalum ya mchezo huo inayoendelea wilayani Ilala jijini Dar es Salaam.
Klabu zingine zitakazopambana katika michezo itakayofanyika mwishoni mwa wiki hii ikiratibiwa na taasisi ya Kinyogoli Foundation ni Ashanti, Big Right na zingine ambazo hazikuweza kufahamika mapema.
Mratibu wa michuano hiyo, Rajab Mhamila 'Super D' alisema michezo hio itafanyika Jumamosi kwenye ukumbi wa Panandipanandi, Ilala Bungoni.
Super D, alisema maandalizi ya michezo hiyo yamekamilika ikiwemo vikosi vya timu zote kuendelea kujifua.
Aliwataja baadhi ya mabondia watakaoziwakilisha klabu zao kuwa ni Ibrahim Class, Khalfan Othman, Kassim Sambo na Saidi Ally kwa upande wa Amana, wakati Matimbwa itawakilishwa na Mohamed Matimbwa, Mohamed Muhani, Edson Joviki na Mohamed Kumbilambali.
Kwa upande wa Ashanti, Super D alisema itawakilishwa na mabondia kama Uwesu Manyota, Ramadhani Kimangale, Mark Edson na wengine na mipambano yao itachezwa kwa raundi nne nne kila mmoja.
Aliongeza kwa kutoa wito kwa wadau wa ngumi kujitokeza kuzisaidia klabu shiriki na mabondia vifaa vya michezo na mahitaji yao mengine ili kuwatia moyo wa kuupenda mchezo huo.

No comments:

Post a Comment