STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 13, 2011

Fella akamilisha albamu ya 'Rusha Roho'




MENEJA wa kundi mahiri la muziki wa kizazi kipya nchini la TMK Wanaume Family, Said Fella 'Mkubwa Fella', amekamilisha albamu yake mpya na ya kwanza ya miondoko ya taarab akiipa jina la 'Kunguni' ikiwa na nyimbo sita.
Akizungumza na MIcharazo, Mkubwa Fella, alisema albamu hiyo ambayo nyimbo zake zimewashirikisha wasanii nyota wa muziki huo kama Khadija Kopa, Maua Tego na Isha Mashauzi itaachiwa rasmi mtaani mapema mwezi ujao.
Fella alisema katika kutaka kuitambulisha albamu hiyo ameshafyatua video ya wimbo wa Kusonona, atakayoiachia rasmi Ijumaa wiki hii.
"Nimekamilisha albamu yangu yenye nyimbo sita ambapo mmoja nimeufanyia video na ninatarajiwa kuanza kuusambaza kwenye vituo vya runinga Ijumaa ijayo," alisema.
Alivitaja vibao vya albamu hiyo ni 'Simuachi', 'Midomo Imewashuka', 'Mchakamchaka', 'Sijapopoa Dodo', 'Kimodern Modern' na 'Kusonona'.
Fella alisema ushirikiano aliofanya na wasanii wenye majina makubwa katika muziki huo utasaidia kuibeba albamu hiyo, iliyotangulishwa na kibao cha Midomo Imewashuka kinachoendelea kutamba kwenye vituo kadhaa vya redio nchini.

Mwisho

No comments:

Post a Comment