STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 1, 2012

BASATA yawalilia akina Sharo Milionea

Sharo Milionea enzi za uhai wake





BARAZA la Sanaa la Taifa, BASATA, limetuma salamu za rambirambi na kueleza kusikitishwa na vifo vya wasanii wa watatu wa filamu na muziki nchini vilivyotokea mfululizo wiki iliyopita.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotiwa saini na Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego baraza hilo limesema limepokea kwa masikitiko makubwa misiba ya wasanii hao ambao ni Khaleed Mohammed 'Mlopelo', John Maganga na Hussein Mkiety 'Sharo Milionea'.
BASATA limedai kuwa vifo vya wasanii hao ni pigo kubwa kwa familia, ndugu, jamaa na wadau wote wa tasnia nzima ya sanaa nchini kwa kusema inaungana na wote walioguswa na msiba huo.
“Baraza limestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa ya vifo hivi vya wasanii hawa John Mganga, Mlopelo na Hussein Mkeity a.k.a Sharo Milionea ambao mchango wao unahitajika sana katika tasnia ya sanaa, pengo waliloliacha ni kubwa kwani ubunifu wao bado unahitajika katika tasnia hii.” Sehemu ya taarifa hiyo inasomeka hivyo.
Taarifa hiyo ikaongeza kuwa; " Baraza linatoa pole kwa familia za marehemu na wasanii wote nchini, aidha linawatakia moyo wa subira katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na wapendwa wetu. Tunaomba mwenyezi Mungu azipumzishe mahala pema peponi roho za marehemu.
BASATA likaongeza kuwa wapo pamoja na familia za marehemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, tutambue kuwa haya ni mapenzi ya Mungu.
Salamu hizo zimekuja wakati watanzania wakiendelea kuomboleza vifo vya wasanii hao pamoja na kile cha muimbaji wa taarab wa kundi la TOT -Plus, Mariam Khamis 'Paka Mapepe' kilichotokea wiki tatu zilizopita wakati akijifungua mwanae wa pili.
Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego


No comments:

Post a Comment