STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 11, 2013

TFF YAMLILIA ATHUMANI KILAMBO

Athuman Kilambo (wa kwanza kushoto waliosmama) enzi za uhai wake akiwa na kikosi cha Pan African miaka ya 1980

Na Boniface Wambura 
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Yanga, Pan Africans na Taifa Stars, Athuman Kilambo kilichotokea jana usiku jijini Dar es Salaam.
Msiba huo ni mkubwa kwa wadau wa mpira wa miguu kwani kwa nyakati tofauti Kilambo akiwa mchezaji, na baadaye kocha alitoa mchango mkubwa kwa timu mbalimbali alizochezea na kufundisha zikiwemo Pan Africans na Cargo, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima.
TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Kilambo, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na klabu ya Pan Africans na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Maziko ya kocha huyo aliyeinoa Pan tangu mwaka 1975 hadi 1984 akiisaidia kutwaa ubingwa wa Tanzania mwaka 1982 na kutetesha soka la Afrika yalifanyika jionio ya leo kwenye makaburi ya Kisutu mkoani Dar es Salaam ambapo TFF imetoa ubani wa sh. 100,000.
Marehemu Kilambo amefariki kutokana na kusumbuliwa kwa muda na ugonjwa wa Kansa ya Koo na inaelezwa marehemu ameacha watoto watano, watat wa kiume wakiwemo nyota wa zamani wa Yanga na Reli Ramadhani Kilambo na Athuman Kilambo.
Mungu aiweke roho ya marehemu Kilambo mahali pema peponi. Amina 

No comments:

Post a Comment