STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, October 18, 2013

TFF bado ina kinyongo na Shafii Dauda yamchinja, ikitangaza majina wagombea uchaguzi mkuu, mwenyewe adai hakubali

Shafii Dauda 'Tishio' akiwa kwenye shughuli zake za habari
 KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imetangaza orodha ya mwisho ya wagombea wa uchaguzi wa TFF na wa Bodi ya Ligi (TPL Board) utakaofanyika baadaye mwezi huu, 'ikimchinja' tena Shafii Dauda katika kinyang'anyiro hicho.
Uchaguzi wa Bodi ya TPL utafanyika Oktoba 25 mwaka huu wakati ule wa TFF utafanyika Oktoba 27 mwaka huu. Kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa TPL Board na ule wa TFF zimeanza leo (Oktoba 18 mwaka huu)  zitamalizika siku moja kabla ya uchaguzi saa 10 kamili alasiri. Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Hamidu Mbwezeleni amewataja wagombea kwa upande wa TPL Board kugombea uenyekiti ni Hamad Yahya Juma (Mtibwa Sugar), Makamu Mwenyekiti ni Said Muhammad Said Abeid (Azam). Wanaowania ujumbe wa Bodi ya Uendeshaji ni Kazimoto Miraji Muzo (Pamba) na Omary Khatibu Mwindadi (Mwadui).
Wagombea kwenye uchaguzi wa TFF ni Athuman Jumanne Nyamlani na Jamal Emily Malinzi (Rais), Imani Omari Madega, Ramadhan Omar Nassib na Wallace Karia (Makamu wa Rais).
Kwa upande wa wajumbe wa Kamati ya Utendaji ni Kalilo Samson (Kanda namba 1- Geita na Kagera), Jumbe Odessa Magati, Mugisha Galibona, Samwel Nyalla na Vedastus Lufano (Kanda namba 2- Mara na Mwanza), Epaphra Swai na Mbasha Matutu (Kanda namba 3- Shinyanga na Simiyu).
Ali Mtumwa, Elley Simon Mbise na Omar Walii Ali (Kanda namba 4- Arusha na Manyara), Ahmed Idd Mgoyi na Yusuf Hamis Kitumbo (Kanda namba 5- Kigoma na Tabora), Ayubu Nyaulingo na Blassy Mghube Kiondo (Kanda namba 6- Katavi na Rukwa), Ayoub Shaibu Nyenzi, David Samson Lugenge, John Exavery Kiteve, Lusekelo Elias Mwanjala (Kanda namba 7- Iringa na Mbeya).
James Patrick Mhagama na Stanley William Lugenge (Kanda namba 8- Njombe na Ruvuma), Athuman Kingombe Kambi, Francis Kumba Ndulane na Zafarani Mzee Damoder (Kanda namba 9- Lindi na Mtwara), Hussein Zuberi Mwamba, Stewart Ernest Masima, Charles Komba (Kanda namba 10- Dodoma na Singida), Farid Nahdi, Geofrey Irick Nyange, Juma Abbas Pinto, Riziki Juma Majala) na Twahil Twaha Njoki (Kanda namba 11- Morogoro na Pwani).
Davis Elisa Mosha, Khalid Abdallah Mohamed (Kanda namba 12- Kilimanjaro na Pwani), Alex Crispine Kamuzelya, Kidao Wilfred Mzigama, Muhsin Said Balhabou na Omary Isack Abdulkadir (Kanda namba 13- Dar es Salaam).
Mbwezeleni amewataka wagombea kufanya kampeni bila kukashfu wenzao, kwani Kanuni ya Uchaguzi za TFF toleo la 2013 inatoa fursa kwa Kamati ya Uchaguzi kuwaondoa wagombea wa aina hiyo kwenye uchaguzi.
Aliyekuwa mgombea wa Ujumbe wa Kanda ya 13, Shafii Dauda ametoswa licha ya kulipa faini aliyotakiwa kulipa ndani ya siku tatu na Kamati ya Maadili ya Rufaa.
Akihojiwa muda mfupi uliopita na kituo cha Uhuru Fm, Shafii amesema hakubali hata kidogo na ameshaanza mchakato wa kupeleka malalamiko yake FIFA kwa madai kuna mchezo mchafu amefanyiwa na kamati hiyo ya uchaguzi ya TFF.
Shafii alisema tangu awali kulikuwa na zengwe kwa lengo la kuwabeba wagombea fulani kutetea nafasi zao na dai kwamba hana uzoefu ni sababu tu, lakini alisema hakubali haki yake ipotee bure na Jumapili atakwea pipa kwenda Zurich makao makuu ya FIFA kupeleka mashtaka yake.
Baadhi ya wadau wa soka waliozungumza na MICHARAZO wamedai kushtushwa na maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF wakidai ni kama kutaka kuleta malumbano yasiyokuwa na sababu yoyote.

No comments:

Post a Comment