STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 23, 2010

Vicky Kamata aimwagia sifa hospitali ya Geita


UONGOZI pamoja na watumishi wa hospitali ya mkoa wa Geita, wamemwagiwa pongezi kutokana na ubora wa huduma zao kwa wagonjwa hospitalini hapo.
Pongezi hizo zimetolewa na mshindi wa kura za maoni za Ubunge wa Viti Maalum Mkoa wa Geita, Vicky Kamata, alipozungumza na Micharazo kwa njia ya simu toka mjini humo.
Kamata ambaye alilazwa kwenye hospitali hiyo kumuugua mwanae mwenye umri wa miaka minne, alisema huduma wapewazo wagonjwa kwenye hospitali hiyo ni ya kupongezwa.
Alisema tofauti na siku za nyuma huduma zinazotolewa na madaktari na wauguzi wa hospitali hiyo ni za kuvutia na kuonyesha kuboreshwa kwa huduma na kuumwagia sifa uongozi na watendaji hao.
Kamata, ambaye pia ni mwanamuziki wa kizazi kipya, alisema hatoi pongezi hizo kwa kuwa alihudumiwa vema kwa wasifu wake, bali ukweli alioushuhudia kwa wagonjwa wengine ndani ya hospitali hiyo ambao baadhi walisifia pia.
"Kwenye ukweli lazima lisemwe, huduma katika hospitali ya Geita ni ya kuridhisha na inayoonyesha mabadiliko makubwa na ninaupongeza uongozi na watumishi kwa ujumla kwa husuma hizo," alisema.
Alisema mwanae aliyelazwa kwa siku nne kutokana na kusumbuliwa na malaria kali tayari ameshatoka na anaendelea vema.
Kuhusu matarajio ya uchaguzi mkuu, Kamata alisema anaamini CCM itashinda kwa kishindo katika uchaguzi ujao kutokana na kutekeleza ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005 kwa ufanisi wakiwapelekea maendeleo wananchi.
"Japokuwa wapinzani safari hii wanaonyesha kucharuka, lakini bado ushindi wa CCM ni kwa kishindo na kuwaomba wananchi wajitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura na kuelekeza kura zao kwa wagombea wa CCM kuanzia Urais, Ubunge na Udiwani kwa nchi nzima," alisema Kamata.

Mwisho

No comments:

Post a Comment