STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 6, 2010

Extra Bongo kupeleka Vuvuzela Kilosa



BENDI ya Extra Bongo, inayotamba na mitindo ya 'Vuvuzela' na 'Kizigo' inatarajiwa kwenda kusherehekea Sikukuu ya Krismasi na wakazi wa Kilosa watakapoenda kufanya onyesho wilayani humo.
Extra Bongo inayomilikiwa na mtunzi na muimbaji mahiri nchini, Ally Choki, itaenda Kilosa kufanya onyesho siku ya sikukuu hiyo kwenye ukumbi wa Babylon Luxury Pub.
Meneja wa ukumbi huo, Robert Chipindula, aliiambia MICHARAZO, kwa muda mrefu wamekuwa wakiombwa na mashabiki wa muziki kuwapelekea bendi hiyo ya Extra Bongo na ndio maana wameialika kwenda kutumbuiza wakati wa sikukuu hiyo.
Chipindula, alisema tayari wameshamalizana kila kitu na uongozi wa bendi hiyo na kukubali kutua wilayani humo kwa onyesho hilo litakaloenda sambamba na utambulisho wa nyimbo na miondoko mipya ya bendi hiyo.
Extra Bongo iliyokuwa ikifahamika kwa miondoko ya Kujinafasi Next Level kwa sasa inatamba na mitindo yao mipya miwili ya Kizigo na Vuvuzela, ambayo wamekuwa wakiitambulisha kila wanapoenda kufanya maonyesho katika maeneo mbalimbali.
Bendi hiyo inayotamba na albamu yao mpya ya Mjini Mipango, tayari imeshaanza kufyatua vibao vipya kwa ajili ya albamu ya pili, baadhi ya nyimbo hizo ni Nguvu na Akili na Neema ambazo zimekuwa zikiwachengua mashabiki wa muziki wa dansi kila zinapopigwa ukumbini.

No comments:

Post a Comment